Monday, October 29, 2007

Soggy Doggy dabo dabo

SOGGY Doggy ambaye amekuwa kimya kwa kipindi kirefu amesema ameamua kuachia nyimbo mbili mpya kwa mpigo ili kujenga heshima na hahofii chochote.

Msanii huyo hajavuma mwaka huu baada ya kukaa kando ya fani hiyo na kujihusisha zaidi na shughuli za utangazaji.

Alimdokeza mzee wa kutibua kwamba nyimbo hizo ambazo ni ‘ICU’ na ‘My baby’ zipo katika ubora mzuri na amezitoa kwa makusudio maalum.

“Hakuna msanii ambae ameshafanya kitu kama hicho nataka nianze kwa mara ya kwanza, wale wa kujirusha hii ya ‘My baby’ ndio saizi yao iyo nyingine imetulia kidogo.
“Ni nyimbo ambazo zina utofauti sana kwa vile nimezifanyia kazi muda mrefu wakati nilipokuwa sisikiki, zipe muda kidogo nizisambaze baada ya wiki mbili utaskia makali ya Soggy yule yule,”alisema msanii huyo.

No comments: