Friday, October 19, 2007

Rooney na Yona Ndabila wa Tukuyu

WASHKAJI zangu inakuwaje kuwaje hapo...! Ishu za 'saa ya inzi na teke la gia' zikoje? Jamaa waliomwendea hewani Mzee mzima wikiendi iliyopita walimpa maripoti ya kumwaga.

Kuna miguno lukuki ya kichinichini, wanangu fulani wanasema wanaskilizia maumivu kutoka na matanuzi ya Idi, masimbi yametoweka ghafla mifukoni na mizinga ndio kibao ili mradi huko Samora na Kariakoo kuendeke watu wakasake lami.

Ndio ukubwa huo…, jamaa wa ukanda wa Oldonyo Lengali wanakuambia "imekula kwako full arifu" .
Wikiendi kama hii, iliyopita ni ya neema kwa Mzee mzima wa kutibua kwenye mambo ya minuso kwa vile alikuwa amejikita kwenye viwanja fulani vya wateule kwa mialiko maalum , ni mitaa ya pembezoni mwa jiji la Kandoro. Mambo ya kuzama midomoni yalikuwa si ya kitoto hapo. Siunajua tetemeko la watu wazima wakivamia fani zao?

Mzee wa Kutibua alikuwa akijipongeza na washikaji zake ambao walifanikiwa kukazia mpaka mwisho, ingawa baadhi kwa taaaaabu na ushahidi anaona kwa vile si mara moja aliwakumbana kwenye viepe wakijiita Philipo badala ya Salehe au Ojuku. Wala huyu jamaa aliyekuja kubanana na mimi hapa kushoto kwangu sijamtaja.

Kiwanja alichoibua wa Kutibua kama kawa kilikuwa na mtu kibao zilizopiga mijusi ya kufa mtu, kila mteule alikuwa akifyonza kwa upana wa domo lake mwanangu na sura fulani fulani zikiwa za hao wanabongofleva pia.

Wakati watu wazima wakiendeleza makamuzi kimtindo, Mzee wa Kutibua akaanza kukumbuka misemo ya waliopiga buku longi taimu huko lasti yiazi kwamba ukitaka kupata nyeti za mtu mzima mtwange kilauri kifike mahala pake.

Jinsi taimu zilivyokuwa zikiyeyuka kauli za wale mlioita Wahenga zikaanza kuthibitika 'laivu' baada ya waliokuwa wakijifanya wapole kuanza kucharuka kwa kutoa stori za kila sampuli.
Si baadhi yao wamezoea maji ya machungwa Stiazi? Mmoja aliyekuwa amenyonga mjusi wake ambao anadai kauibua dukani huko Samora kwa jiwe kadhaa kashauvua kaupiga mezani na shati alilokuwa akilinadi kanunua kilo limechomolewa saidi moja linaning'inia.

Kando kando waliobana na kina mamananihii wao tayari wameanza kupata burudani kwani mwanabongofleva (tumsitiri kwa jina) mmoja ambaye ni swahiba kinoma wa Mzee wa Kutibua ameshaanzisha tafrani ambayo hata fidifosi wa bwana Mwema hawaiwezi, si maji yamevamia oblongongata!

Kalipua bomu kwamba amempiga kitambi waifu wa mshikaji mmoja ambaye ni miongoni mwa wawezeshaji wa mchakato wa Bruwarizi kwenye hiyo mitingi inayoendelea, jamaa kusikia kukachafuka huku wazee wa udaku wakinyemelea kando kando kutaka kunasa hili na lile.
Mzee wa Kutibua ambaye ni muoga wa manundu ya kujitakia, mida hiyo yuko na nanihii zake kadhaa kichwani, kashapotea kwenye uwanja wa mapambano ili kuwaacha walioshiba watengenezane na hata ikiwezekana baada ya siku tuskie singo mpya imetoka kwa ‘Bonyeza’ hapo Morocco au kwa ‘Matawi’ Mikocheni. Ndio inavyokuwa kwa wanabongofleva wenu! Unashangaa….. kwani hujaskia huyo aliyetunga eti “yuko Bar wife asimtafute”! Huwaiiii…?

Labda tuchenji chaneli. Lakini hivi kama mnataka ndondi simuingie gyimu mmalize kazi tuwaunganishe kwenye listi ya Matumla na swahiba yake Cheka? Ndio maana yake kwani sisi tumewaambia uwanjani tunakuja kuangalia ngumi sisi!

Mmepewa vichwa mkapitiliza sasa mmeamua kugeuza na uwanja wa soka sehemu ya mapambano baada ya kuona mambo yamekuwa mazito.

Upuuzi huo wa baadhi ya wachezaji wakiongozwa na hao wa hizo zinazoitwa Simba na Yanga umekuwa ukijitokeza kwa kiasi kikubwa katika wiki chache zilizopita ambapo bila ajizi na waamuzi nao wamekuwa wakigawa redi kadi na yello kama njugu, kitu ambacho pia kimekuwa kikichanjia kuharibu ladha ya Ligi Kuu hii ya Bara.

Utovu wa nidhamu kwa wachezaji sasa umeonekana kupitiliza kutokana na kutofuata taratibu, kanuni hata sheria zilizowekwa. Au ukisajiliwa ukipewa Baluni na geto la chumba kimoja tena uswazi ndio umefika mwisho kila kitu kipo chini yako? Ni dalili za kuchuja kama hamjui masela.

Sifa za kijinga za uwanja wa Jamhuri au Taifa hazikusaidieni, badilikeni mcheze soka kwa kutuliza mpira chini na kufuata maelekezo Nainte minitsi, utovu wa nidhamu na ukorofi hausaidii.

Haya mangumi uwanjani, kupigana hovyo, matusi na kuumizana bila sababu za msingi hakuwajengi, hakuna anayekwenda uwanjani kuangalia nani atamkunja nani au nani mbabe wa nani, tunataka kuona futiboli badilikeni mtushawishi angalau tuanze kufikiria kuachana na hao wa kina Rooney na Terry wa England tumuangalie Yona Ndabila wa Tukuyu. Kwani wana tofauti gani?

Mwenye akili timamu ataelewa anachonena Mzee wa Kutibua, hayo mambo ya ubabe waachie hao wanaoitwa makomandoo wapambane na wanaowajua wao kusaka hizo buku za geti koleksheni!

Hata propaganda za kiuongozi haziwahusu kabisaa…, kazi ya mchezaji ni kucheza soka ili mradi uwe unalipwa kilicho halali yako vijana na mama nanihii apige viwalo vya maana.

Wala suluhisho la kuboreshewa maslahi au kutekelezewa mambo yenu si kwa timu kufungwa au kutoa sare, mwisho wa siku nyie wachezaji wenyewe ndio mnajiharibia, viongozi ni watu wa kupita tu leo na kesho hawapo nyie timu ikiboronga nap engine kushuka daraja wakala gani atakuangalieni? Au atakayeelewa sababu zenu za Kiswahili eti kwamba mlitibua ili Mwaisakandu atimuliwe na wanachama.

Soka ni laifu yenu wanangu na mnapaswa kulisukuma kiukweli, hamkereki na hivyo vikwapa vya makonda, ifike mahali na nyie mjitume zaidi muishi maisha mazuri na mkwee huko ughaibuni wanakovuna dola wenzenu.

Kubalini kubadilika kifikra na muangalie wanachofanya wenzenu walioendelea, wanangu mjenge utamaduni wa kujifunza na kwenda sambamba na mabadiliko ya huko ‘Duniani’.

Hata Marefa na wenyewe wanapaswa kuwa makini zaidi kuepusha ndondi na rapsha baina ya wachezaji bila sababu za msingi na ambazo zinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kuvuruga saikolojia na kuharibu mchezo.

Zingatieni sheria na muwe makini zaidi si kugawa kadi ili mradi tu. Siyo kwamba hatujui, tunajua mpo mnaovuta mapene na kupindisha mambo tumeshawapa tipu Takukuru wako mitaani.
Ayaaah….! kabla sijaingia mitini! Wanangu wa mji kasoro Bahari, Jeitano nipo ndani ya stadiumu kushuhudia watu wazima mzigoni, mwisho na mwanzo wa ubishi mpya. Mwekundu au Wanjano atacheka? Kazi kwao!
Haluu...! linakuja Libulogi la Mzee wa Kutibua ni funika bovu, Bongo nzima hakuna! unaweza ukalichungulia hata mida hii kama vipi (mzeewakutibua.blogspot.com) lakini kuwa mpole linasukwa na wanazuoni wa hapo Mlimani.

No comments: