Wednesday, March 26, 2008

Sitaki kabisa hii aibu wala msiniambie!


UKITAKA kuinjoi Bongo basi siku kama hizi za minuso ya sikukuu ndio freshi za kuibuka.
Ndio maana Mzee wa Kutibua hukumbwa na malaria za ghafla pamoja na kuhara kusikoisha ilimradi tu kupata visingizio tosha mpaka wiki ijayo asiibuke kazini.
Nani asiyejua utamu wa tumbo la kuhara bwana...? kumbe mzee mzima niko zangu kwa 'wenyenchi' nkivunja mbavu na kushuhudia viroja.
Ndio nyakati murua ambazo kumfuma mheshimiwa mzima amekwidwa shati na waifu mida ya asubuhi baada ya kuwa bwaksi wala siyo ishu saana Uswazi.
Si alilala kaunta halafu homu ya vitumbua hajaacha?
Kumbe Jumamosi kama hii ya Shopingi ya Pasaka pia ndio wajanja ambao baadhi wamekwenda mbali zaidi kwa kuchongesha suti zao mithili ya maafisa wa benki hujazana Kariakoo na Mnazi Mmoja utafikiri mashushu wa mafisadi.
Wala hakuna cha mashushu ndio staili mpya ya wakwapuaji wa Dasilamu, Bongo kuna mambo!
Kaa naye vibaya halafu akikutoka viwalo vyako spidi atakayochomoka nayo ndio utajua kweli mjini shule.
Ndio mambo ya tawni, we unafikiri ni wote walioulamba unaopishana nao huko katikati ya Jiji wakimwagika jasho wametoka kula vyuku Stiazi?
Watu wako kwenye mishemishe ukizubaa kidogo wakikuingia anga zako ndio umeumia.
Lakini ebu tuache kwanza hizo, hivi kweli hawa jamaa zetu wa hiyo kamati mnayoita ya mashindano wanataka kutupeleka wapi? Mchezaji anamsukuma mwenzake wanamfungia mechi sita za ligi? Wati izi disi!
Unashangaa.. kwani hujaskia yaliyomkumba Emmanuel Gabriel wa Simba wiki iliyopita? Gabriel(pichani) alifungiwa baada ya kutenda kitendo hicho kama mechi dhidi ya JKT Ruvu mjini Arusha.
Lakini kanuni gani hizi zinazotuongoza, mbona huko Ulaya kwenye wenzetu walioendelea tumekuwa tukishuhudia hayo mambo kila siku.
Mara ngapi tumemshuhudia Emmanuel Adebayor wa Arsenal, Jermen Pernant wa Liverpool, Wayne Rooney wa Manchester au hata Joe Cole wa Chelsea wakifanya makosa kama hayo lakini huwezi kusikia kafungiwa mechi sita zaidi ya kuitwa na kuonywa? Hizo adhabu ni kwa manufaa ya nani? au ndio kukomoana tu ili mradi?
Ambacho nilitegemea labda mwamuzi wa ule mchezo Arusha angewaita wote wawili pale pale uwanja na kuwaonya na kama ingezidi sana mmoja wao angepewa kadi ya njano. duh! hii kiboko.
Hilo lilinikera sana nikaamua niliseme kwanza. Lakini kubwa ninalotaka kusema Jumamosi hii ni kwamba hatutaki aibu washikaji, kila kitu mnacho.
Timu ya soka ya Taifa Stars imepangwa kuanza na Kenya Machi 30 kwenye michuano ya kuwania kufuzu Afrika inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za ndani,tunaanzia Nairobi wala hiyo siyo sababu. Kocha wa Stars Marcio Maximo ameshatangaza kikosi chake chenye wachezaji wengi wenye uzoefu mkubwa na ambacho kesho Jumapili kinatinga kambini.
Nimekuwa na imani na kikosi kilichotangazwa pamoja na benchi la ufundi lakini tatizo langu bado lipo kwa wachezaji wenyewe binafsi.
Wachezaji wengi wamekuwa wakichaguliwa wanapoingia Stars wanashindwa kufurukuta huku baadhi wakidai uzoefu na kubaniwa na kocha vinawasumbua. Wengine wanaotoka timu za mikoani wameenda mbali zaidi na kusingizia hali ya hewa.
Ukikaa na kupiga stori na wachezaji walioitwa kwenye vikosi vilivyopita ndio mambo mambo waliyokuwa wakieleza lakini ukiingiza kwenye akili za kawaida hata bila kushtukia(mambo yetu yalee...) jibu la haraka linakuja ni uvivu na kutojielewa.
Wadau wamemwaga manoti kuhakikisha Stars inasonga mbele katika mashindano ya sasa baada ya mwaka jana kushindwa kufuzu kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika yaliyofanyika Ghana.
Wachezaji wanaishi kwenye hoteli ya kifahari kama kawaida, wana basi la kisasa la mamilioni ya shilingi tena lenye kiyoyozi, vifaa vya kutosha, posho tena za kiwango cha juu na kila kitu anachostahili mchezaji.
Sina wasiwasi wala sitaki kuchunguza uwezo wa makocha Wabrazili waliopo lakini wachezaji wanapaswa kufungua akili na kujua kwamba huu ndio wasaa pekee wa kuonyesha makali yao.
Soka ni ajira yao si sehemu ya kufanyia starehe au kujipatia umaarufu. Kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa kuheshimu nafasi aliyopewa na Maximo na kufanya kazi kikamilifu kwa kutoridhika wala kuvimba vichwa kipuuzi na kupandisha mabega.
Mna kila kitu na sababu tosha za kutufanya tucheke safari hii tumechoka kununa na kuangalia kina Drogba, Ronaldo, Fabregas kwenye video.
Acheni uzembe fungueni akili na muelewe maelekezo mnayopewa ndio kitu pekee kinachoweza kuwafanya mwende huko kwenye mikwanja mikubwa wanayovuta wenzenu 'wa ukweli'.
Kenya haina kikosi cha wachezaji wa ndani watakaotusumbua hivyo, mna uwezo wa kutoa sare kwao au hata kushinda ambayo ndio matokeo tunayohitaji ili kazi iwe rahisi tuwamalizie Nashno Stadiumu tumlie taimingi anayekuja.
Acheni uvivu, tulizeni akili uwanjani muuonyeshe umma kwamba Tanzania inaweza na ina vichwa vinavyolitandaza soka la ukweli ambavyo havistahili kuishia uswahili.
Hakuna cha ajabu. Hii ndio nafasi pekee ya kuchanua Afrika na wachezaji kujijenga na kujiuza nje ya nchi. Tuna kila sababu ya kucheza fainali za Ivory Coast mwaka huu tupambane na waswahili wenzetu jamani tunawaweza kabisa.
Oyaa.. washkaji eee kazeni buti. Wanangu wa Moro kesho siunajua mwanetu Afande Sele anachanga changa karata Dume hapo Mambo Club? Full kujiachia..Tuibuke basi kimtindo Mzee mzima nitakuwemo na wanangu kibao...Siunajua mambo yetu yalee..
0713-374649
momburi2002@yahoo.co

Afande sele noma..! we acha tu.


Afande Sele aikamata tena Morogoro
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
KAMA ilivyotabiriwa awali, Afande Sele kwa mara nyingine juzi usiku alifunika kwenye uzinduzi wa albamu yake ya 'Karata Dume' uliofanyika kwenye ukumbi wa Mambo Club mjini hapa.
Msanii huyo ambaye ni kipenzi cha mashabiki wengi wa hapa, amekuwa na rekodi ya kufanya vizuri kwenye zinduzi zake tatu zilizopita kama ilivyokuwa juzi mbele ya mamia ya mashabiki waliofurika kwenye ukumbi huo.
Si Afande tu wasanii waalikwa kama Jua Cali wa Kenya alifunika na wimbo wake wa 'Kwaheri' huku AY, Dully Sykes, Jaymo na Bwana Misosi nao walikonga nyoyo za mashabiki.
Wasanii Ditto na MC Koba waliorejea kundini hivikaribuni baada ya kupatanishwa na Afande, waliwapagawisha mashabiki walipoimba nyimbo zao za zamani wakati wakiwa kwenye kundi la Gheto Boys.
Afande ambaye alipanda jukwaani majira ya saa nane usiku, alipagawa na makelele ya mashabiki wakati alipoanza kuimba wimbo wake unaovuma wa 'Karata Dume', akavua Jinsi na fulana yake na kubaki na bukta na vesti.