Wednesday, March 26, 2008

Afande sele noma..! we acha tu.


Afande Sele aikamata tena Morogoro
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
KAMA ilivyotabiriwa awali, Afande Sele kwa mara nyingine juzi usiku alifunika kwenye uzinduzi wa albamu yake ya 'Karata Dume' uliofanyika kwenye ukumbi wa Mambo Club mjini hapa.
Msanii huyo ambaye ni kipenzi cha mashabiki wengi wa hapa, amekuwa na rekodi ya kufanya vizuri kwenye zinduzi zake tatu zilizopita kama ilivyokuwa juzi mbele ya mamia ya mashabiki waliofurika kwenye ukumbi huo.
Si Afande tu wasanii waalikwa kama Jua Cali wa Kenya alifunika na wimbo wake wa 'Kwaheri' huku AY, Dully Sykes, Jaymo na Bwana Misosi nao walikonga nyoyo za mashabiki.
Wasanii Ditto na MC Koba waliorejea kundini hivikaribuni baada ya kupatanishwa na Afande, waliwapagawisha mashabiki walipoimba nyimbo zao za zamani wakati wakiwa kwenye kundi la Gheto Boys.
Afande ambaye alipanda jukwaani majira ya saa nane usiku, alipagawa na makelele ya mashabiki wakati alipoanza kuimba wimbo wake unaovuma wa 'Karata Dume', akavua Jinsi na fulana yake na kubaki na bukta na vesti.

No comments: