Friday, February 22, 2008

Huu wa Arsenal Wenga ni ukoloni


EBWANA wanangu inakuwaje? Ishu zinaendaje mitaa ya kati hapo, shukrani sana kwa kukodolea macho mitaa hii linakomwaga sera Zee la Kutibua.
Mwanenu lasti wiki ishu zilikuwa nuksi kichizi, mijicho ilikuwa haitaki kuona mambo fulani.
Jamaa zangu fulani ambao hawajaaga Mpwapwa kama Mzee wa Sumo wanaweza kufungasha virago wakidhani ni pua ya mtaalam inafanya mambo yake.
Unafanya mchezo nini? Yaani Red aiyizi noma nakwambia, hata wakaanga sumu macho yao yana nafuu.
Lakini shwari kimtindo Mzee mzima sasa niko freshi napeta zangu kwenye viunga vya Kandoro ambavyo porojo za kifisadi zimepotea kijiweni na kilichobaki ni simulizi mpaka za buti za Bush.
Si baaada ya Bush kutua na midege yake? Palikuwa hapatoshi wana! Hata wauza mihogo wa mtaani kwetu Vingunguti Kiembe Mbuzi walipiga zao mguu na kuibuka Eapoti kumshangaa mshkaji.
Waliobaki uswahili na wenyewe ni vimbwanga tupu, muda wote mijicho haibanduki angani wakishuhudia mihemko na mbwembwe za midege ‘Eafosi wani’.
Wapo wadeni waliobonyeza Mzee wa Kutibua na kumtonya kwamba ujio wa mshkaji umewasevu pia na kuwapa mwanya wa kupishana milangoni kwani wenye mapango walinogewa na soga na kuhamishia bongo zao skani.
Lakini tukiacha porojo hili la FA kutaka kutulelea ligi yao bongo silikubali. Haiwezekani huku ni kutumaliza kabisa pamoja na kidogo tulichonacho.
Wiki chache zilizopita kamati ya Ligi Kuu ya England ilitoa pendekezo na kuonyesha nia ya kutaka Ligi Kuu ya nchi hiyo baadhi ya mechi zake zichezwe kwenye nchi nyingine Duniani ifikapo msimu wa 2010-11.
Rais wa FIFA, Sepp Blatter ameibuka na kupinga mapendekezo hayo kwa kile alichoeleza kwamba ni kinyume na sheria na kwamba itakuwa ni kuangamiza ligi za nchi nyingine.
Jamaa akaendelea kueleza kwamba itatibua pia kampeni za Weldi kapu 2018. Lakini baada yake Aseno Wenga ambaye ni kocha wa Aseno akaibukia kusikojulikana madai yake ni kwamba Blata kachemka.
Anachosema Wenga ni kwamba ligi iruhusiwe kuchezwa nje ili kutangaza zaidi ligi yenye ushindani, kutoa nafasi kwa mashabiki kufaidi uhondo ikiwemo pia kwa klabu husika kujiingiza mamilioni. Mzee Wenga pamoja na Uprofesa wako na hao jamaa wa FA hatutaki.
Lakini wana hii ishu mi sikubaliani nayo! Tukiwaruhusu wakicheza tu Afrika tumekwisha na ndio mwanzo wa kuuwa kabisa ligi na klabu zetu. FA inataka mechi moja ya mwisho kila msimu kwa kila timu ihamishiwe Afrika, Asia au Amerika.
Kwa hali ilivyo sasa mashabiki asilimia kubwa wanabeza ligi zao za nyumbani na kushabikia klabu za England ambazo wanaziona kwenye kideo. Je zikija kucheza hizo mechi zao moja moja Afrika au kwenye hizo nchini nyingine si ndio watatuuwa kabisa na msisimko wote wa mashabiki utahamia Ulaya na kupuuza ligi zao na wachezaji wao?
Hakuna siri kwamba ligi hata klabu nyingi za Afrika bado ni changa na zinahitaji sapoti kubwa ili kuzipandisha katika kiwango ambacho angalau kitakaribiana na wenzetu walioendelea lakini kwa kuwakaribisha wenzetu watumie ardhi yetu ni kupotea maboya.
Tunapaswa kulinda klabu zetu na ligi zetu sasa, Waingereza wametutawala mno kwa kila kitu haiwezekani watuletee mpaka na ligi yao kana kwamba sisi hatuna thamani. Mbona wao hawasemi zetu zikachezwe kwao?
Najua kwa mashabiki ‘walevi’ wa kina Ronaldo wa Machesta, Fabregas wa Aseno au Lampard wa Chelsii hata Gerad wa Livapulu watafurahia wazo la ligi hiyo kuchezwa nje na kuongezwa hadi 39 badala 38 ili wawaone wachezaji wao lakini hasara zake ni nyingi kuliko faida.
Nani atahangaika na Masumbuko wa Mtibwa,Ulimboka wa Simba,Tegete wa Yanga au Mangunguru wa Moro?
Kama lengo lao ni kuja kucheza na klabu zetu kuzipa uzoefu na kubadilishana baadhi ya mambo sawa, lakini si mje mkacheze wenyewe kwa wenyewe.Hakuna faida kwa hilo kwa nchi kama Tanzania zaidi ya kuuwa kabisa ligi yetu. Waingereza wametuletea teknolojia nyingi za kisasa, wametulazimisha kuiga mfumo wao wa maisha tukaachana hata mambo yetu ya kiutamaduni kwa madai kuwa tunakwenda na wakati sasa wamekaa wamefikiria na ligi zetu za ndani hazina maana wameona watuletea zao? Kwanini tukandamizwe kiivyo, lazima tujifunze kuwa maskini jeuri?
Tusikubali kushikwa masikio kwa kila kitu anachoamua mzungu hata kama ni cha kipuuzi, kwa nini ligi yao wasicheze huko huko kwao?
Muda wa kutawaliwa kifikra umekwisha, walishatukalia miaka ya nyuma na kutuweka mifuko mwao, tukajitahidi tukapata uhuru wetu tusiwakaribishe tena watutawale watatuharibia timu zetu za Taifa.
Si wacheze kwenye viwanja vyao sisi tutawaangalia kwenye kideo kwani lazima waje Afrika? Labda Asia na mabara mengine.
Ni changamoto sasa kuwekeza na kuhakikisha ligi zetu zinapiga hatua kwenda kwenye kulipwa waliko wenzetu na tujitahidi kujifunza zaidi kila kunapokucha na tusikubali kuendeshwa na wakubwa kana kwamba sisi hatuna akili wala ujuzi wa kupanga mambo yetu, huu ni ukoloni wa waziwazi.
Mzee wa Kutibua anatia zake nanga mitaa hii, lakini wana..tuibukeni Taifa tukawapige tafu dada zetu wa Twiga Stars, wanatisha kinoma si umeskia leo wanakipiga na mademu wa Kameruni? Tuibuke halafu badaye kama kawa Mugongo...Mugongo..!
Wengine Samaki ana vipande vingapi..!
0713374649
HYPERLINK mailto:momburi2002@yahoo.com
Mzeewakutibua.blogspot.com

No comments: