Saturday, February 16, 2008

Atanyongwa mtu nakwambieni...

MASELA wengine nuksi tu, aheri hata wangebadilishwa na Magunia ya mkaa tukajua moja tu.Bora tu kwani ni nini bwana? Tena laifu ingesonga tu kiulaini kinoma.
Tunawekeana viwingu viwingu vya kizushi bwana laifu lenyewe lipi bwana kibongo bongo na mwendo wetu wa Daladala.
Longolongo nyingi halafu wanatutibulia ishu zetu tu, utafikiri virusi bwana! Kila ukitulia kwenye engo yako unakula zako ‘Uwele’ na wajisiriamali mkipanga mishemishe za hapa na pale wamo, wameibuka na vijimambo vyao, inakuwaje kiivyo wana? Au kuweka maskani ya muda Shamba imekuwa nongwa?
Mara oooh..Mzee mzima hongera bwana nimeona jana waifu katuletea kitu kipya mtaani bwana...
Bado jamaa zinaendelea tu, nkafikiri labda shida ni kilauri nikawachapa moja moja ili wasepe na ishu zao. Bwana si wakazidi kumwaga umbea bwana...? Mara oooh... nimeskia jamaa unamuoa tena nanihii bwana inakuwaje mbona hivyo...!
Si wakazidi kuniganda bwana...mpaka wakaniachia Redi Aizi rafiki yangu. Naiti naibuka homu mambo si yakaanza kujibu yaani noma tupu, mzee mzima nimeumbuka mchana kweupee.. jicho halifai. Au kuna pua ya mtu nini Masela?
Waliomshtukia Mzee wa Kutibua akinyatanyata kwenye korido za tabibu fulani mitaa ya Kinondoni wakamuibukia na kumshauri eti anawie mkojo wa mademu ishu itakata fasta. Eh! Si wana watanikimbia Bongo? Haiwezekani hiyo wakubwa.
Lakini ishu zinasonga ingawa mambo si mambo kwenye waleti za wanangu fulani ambao kupiga mguu siku kama hizi kukatiza mitaa ya Kino kuibukia Dasilamu mjini ni ishu ya kawaida.
Ndio maisha ya bongo hayo, usione jamaa linamwagika jasho ukafikiri ni misosi imekubali. Mambo yametaiti kila kona, nani arudi Itigi aiache Samora Avenyuu Darisalamu. Unacheza... nini!
Ebu ngoja kwanza nkupe ishu! Hawa wababaishaji wanaojifanya wanazipenda timu zao wakiendelea kuendekezwa kwenye uwanja wa Taifa, iko siku watanyonga mtu na mtalia.
Tiefuefu na Polisi fungueni macho, Musiwe wanafiki hivi vitendo vinavyofanywa na mashabiki wa Pan Africa na majirani zao wa Ashanti ni hatari kwa maisha ya binadamu.
Tumekuwa tukishuhudia katika mechi zinazohusisha timu hizo mashabiki wenye jazba wakisogelea mabenchi yao ya ufundi mara kadhaa na kutukana na kutishia makocha na wachezaji.
Baadhi wamekuwa wakikera wachezaji na kuwapotezea umakini wa kusoma na kuangalia kwa kusimama kwenye uzito karibu na mabenchi na kuwatishia.
Lakini cha kusikitisha zaidi tumeshuhudia wengine wakipenya uzio kwa kupitia kwenye geti kubwa kwenda mpaka kwenye benchi kutishia kwa maneno makocha huku wakiwaelekeza kufanya mabadiliko? Nini kazi ya hao Polisi getini?
Vitendo hivyo ambavyo vya kibabaishaji, vinavyofanywa na baadhi ya mashabiki ambao sisiti kusema ni wababaisha ni vya kudhalilisha taaluma kwa makocha husika na kuvuruga wachezaji.
Napata ugumu kuelewa upeo na wanachofikiria viongozi wa klabu hizo ambao kwa mara kadhaa tangu vitendo hivyo vimekuwa vikionekana kwenye uwanja wa Taifa sikupata kusikia au kuona wakitamka chochote. Msafiri vipi bwana! Au ndio kawaida Ki-Ilala Ilala?
Haiwezekani shabiki tena Mzee wa miaka isiyopungua 60 anatoka jukwaani huku akishangilia na wanazi wengine anapenya uzio ulio chini ya Polisi na kwenda kuwafokea makocha kwenye benchi huku ngazi zinazohusika kila mmoja akishuhudia.
Akienda na silaha akamchoma kocha au mchezaji je?Nani atawajibika kwenye hili na ni uzembe wa nani?
Kwanini kila mtu asipewe nafasi na kutekeleza majukumu yake kiufasaha? Hawa wababaishaji wataendekezwa mpaka lini. Kwanza wana mchango gani kwa klabu zaidi ya kujitokeza tu na kuanza kupiga makelele uwanjani, unazi gani huo wa kishamba wakubwa?
Viongozi wa hizi klabu za Ashanti na Pan Africa wanapaswa kuwaelemisha na kuwadhibiti mashabiki wao. Hata Tiefuefu inapaswa kushikilia makali zaidi kwa kuhakikisha kila mtu anakuwa huru kutekeleza majukumu yake na wababaishaji wanaojifanya wana machungu wadhibitiwe na sifa za kijinga ziwaishe.
Haiwezekani watu wenye ‘mamulhaka’ tukalea vikundi vya mashabiki wachache wanaotaka kutuvuruga na kutupotezea uelekeo. Hawana jipya na naamini hata fomesheni pengine hawajui kabisa. Kwanini tunalea uozo kama huu?
Ebwana wanangu eee... naingia mitini kimtindo. Mwanangu Uli, Machupa ...ee..kesho vipi Taifa hapo? Mshkaji wangu Ben, Ngassa...ee inakuwaje Madagasca hapo itakuwaje?
Sasa ni intaneshno mechez kuanzia kesho. Simnajua? Tuache unazi wa kishamba, tuweke mbele uzalendo tushangilie Wanaume wasonge mbele.
Utani sio uadui... achaneni na ushabiki wa mwaka Arobaini na saba mbona mabosi wenu wanakaa meza moja hamuoni hata hao wazungu wanapiga kinywaji pamoja?
Bofya basi kwenye MZEEWAKUTIBUA.BLOGSPOT.COM utaliona laivu zee la Kutibua. Badae kama kawa Kungwasumika Keinyama au Kupekecha Msasani. Redi Aizi kitu gani bwana?ntaibuka we ncheki maeneo maeneo hapo ila tusikerane.
0713374649

No comments: