Sunday, February 17, 2008

Makocha wa Yanga wampa Umbea Milovan


MAKOCHA wa Yanga, Kondic Dusan na Spaso Solokovisk (kwenye picha) wamemweka kitako na kumueleza kila kitu kocha mpya wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic.

Milovan alitua nchini wiki iliyopita alisaini mkataba wa mwaka mmoja na Wekundu hao kwa mujibu wa Mwenyekiti wa klabu hiyo, Hassan Dalali. Katika mechi ya Ligi Kuu ya Bara, baina ya Prisons na Manyema juzi kwenye uwanja wa Taifa, Kondic, Spaso na kocha wa vijana wa Yanga, Zivojnov Srdan walimchukua kocha Milovan na kukaa nae zaidi ya dakika 25. Prisons ilishinda 4-1.

Hali hiyo ambayo iliwashangaza baadhi ya viongozi wa klabu hizo ambao ilibidi waduwae kwa vile si jambo la kawaida katika miaka ya hivikaribuni kwa makocha wa timu hizo hasimu kukaa na kubadilishana mawazo kwa muda mrefu.Tukio hilo ambalo lilitokea kwenye jukwaa la wageni wa heshima (VIP) wakati wa mapumziko ya mchezo huo lilitokana na makocha hao wenye hadhi ya Uprofesa kufahamiana kiundani kwa miaka mingi tangu wakiwa kwao Serbia.

No comments: