Sunday, February 17, 2008

Ronaldo kwisha kazi yake


PARIS, Ufaransa

MSHAMBULIAJI Ronaldo de Lima ameendelea kuandamwa na jinamizi la kuwa majeruhi akiwa na AC Milan baadaye kumia mguu na kufanyiwa operesheni itayomweka nje ya uwanja kwa miezi tisa.

Ronaldo alifanyiwa upasuaji huo katika hospitali ya Pieté-Salpetriere mjini Paris ilo fanyika kwa usalama juzi usiku kwa mujibu magezeti ya Ufaransa. Operesheni hiyo ilifanyika saa 3:00 usiku chini ya Professor, Gerrard Saillant ambaye alimfanyia Ronaldo upasuaji wa goti lake la mguu wa kushoto. Baada ya upasuaji huo daktari huyo alielezea jinsi hali ilivyokuwa ya mafanikio.

No comments: