Thursday, February 21, 2008

Kikwete- Twiga Stars mnaweza komaeni

RAIS Jakaya Kikwete amewataka wachezaji wa timu yasoka ya wanawake Twiga Stars kucheza kwa kujiaminiwatakapopambana na Cameroon Jumamosi, akisema "mnavyoonekana mnaweza"
Rais Kikwete amesema hayo jana Ikulu jijini Dar Es Salaam wakati wa chakula cha usiku alichowaandalia wachezaji wa Twiga Stars kwa ajili ya kufahamiana kwa kuwa hakupata fursa ya kuwatembelea kambini.
Twiga Stars itapambana na Cameroon katika michuano yaawali ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za Mataifa ya Afrika baada ya kuwatoa Eritrea kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2.Fainali za michuano hiyo zinatarajiwa kufanyika Guinea Juni mwaka huu.
Rais alisema: “Mnacheza na Cameroon yenye jina kubwa katika soka la wanaume si wanawake. Hakutakuwepo na Eto’o.
Mtoke hapa muingie kiwanjani mkiamini niko nanyi. Jiaminini na mjue kuwa nyinyi ndio mtakaoshinda na Watanzania wote wako nyuma yenu. Soka la wanawake halina muda mrefu kinachotakiwa ni kujiamini na kuungwa mkono.”

No comments: