Sunday, February 17, 2008

Hichi kijamaa ni noma-Neville


LONDON, England

BEKI na nahodha wa Manchester United, Gary Neville amewatahadhalisha wapinzani wao wa Kombe la FA timu ya Arsenal kuwa waaangalifu na Cristiano Ronaldo(pichani) kwa sababu anacheza soka ya sayari nyingine msimu huu.
Nahodha huyo Neville ambaye amekuwa benchi kwa muda mrefu msimu kutokana na kuwa majeruhi, amesisitiza Ronaldo sasa ni sawa na nyota wengine wa Red Devils, kama Eric Cantona, Roy Keane na David Beckham.
Neville, 32, alisema: “Katika suala kuburudisha, kutegeneza na kufunga, utapenda kumuona mchezaji huyu akiwa na mpira. Ni mchezaji wa kutoka sayari nyingine.”

No comments: