Sunday, February 17, 2008

Ujasiri wa kufumba macho


LICHA ya kukosa mechi za kimataifa za kujipima nguvu, Kocha mkuu wa timu ya soka ya taifa ya wanawake 'Twiga Stars' Charles Boniface amesema kikosi chake kina mabadiliko makubwa kiuchezaji.
"Naona sasa kuna mabadiliko kiuchezaji lakini kikubwa ni kuanza kujiamini, wachezaji sasa wanajiamini kutokana na kuondoa woga ni mambo madogo tu ya kitoto bado tunajaribu kuyaondoa," alisema Mkwasa.

Lakini licha ya matizi ya kufa mtu yanayopigwa na hawa vijana kwenye uwanja wa Karume bado wataalam wa mambo wanadai ni ngumu kuifunga Cameroon kwa kucheza na timu za Uswazi na wazee wanaotokea Bar kwenye mazoezini.

No comments: