Thursday, February 21, 2008

Hii ya Simba ni hatari kubwa


Timu ya Simba imelazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar na kufikisha pointi 24 ambazo ni hatari kwake kwani katika mechi iliyopita ilitoa suluhu na Manyema United inayokaribia kushuka daraja.

Endapo Simba isipojirekebisha huenda ikampaka faida mtani wake Yanga mwenye pointi 33 ambaye akishinda mechi sita tu kuanzia sasa anamvua ubingwa kwa kufikisha pointi 51 kwani Simba ikishinda zote nane ilizonazo kwa sasa itafikisha pointi 48 tu na kuinua mikono juu. Machupa, Ulimboka mpo?

No comments: