Sunday, February 17, 2008

Kanye West afunika Grammy

MWANAMUZIKI wa Uingereza, Amy Winehouse na mzoefu Kanye West ndio waliofunika tamasha kubwa duniani la kutuza wanamuziki la Grammy ambalo lilifanyika Jumapili iliyopita ikiwa ni mara ya 50 tangu kuanzishwa.Lakini wanamuziki hao wawili waliikosa tuzo kubwa ya Albamu Bora ya Mwaka iliyonyakuliwa na Herbie Hancock inayoitwa "River: The Joni Letters", ambayo ni mkusanyiko wa nyimbo za mkali wa nyimbo za jazz, Joni Mitchell (ikiwa na wasanii waalikwa ambao ni wapiga gitaa maarufu kama Norah Jones, Tina Turner, na Corrine Bailey Rae).Winehouse, ambaye alitumbuiza kibao chake cha ''I'm No Good'' na ''Rehab'' kupitia luninga akiwa jijini London, nusura atwae tuzo zote alizotajwa kuwania.

No comments: