Saturday, February 16, 2008

Simba, Yanga zipo kazini


ZIKIWA chini ya maprofesa kutoka Serbia, Simba na Yanga zinaanza rasmi kazi nyeti za kimataifa zitakapokuwa katika viwanja tofauti kesho Jumapili.
Yanga chini ya Profesa, Kondic Dusan na msaidizi wake Spaso Solokovisk ipo mjini Antananarivo, Madagascar kuivaa AS Adema ya huko kwenye mechi ya raundi ya awali ya Kombe la Shirikisho.

Simba ya Mtaalam Milovan Cirkovic ipo kwenye uwanja wa Taifa ikiivaa Awassa ya Ethiopia.

No comments: