Saturday, February 16, 2008

Milovan ampa shavu Julio


KOCHA mpya wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic amekiri kuwa ana kazi kubwa ya kuibadili timu hiyo kutokana na kiwango alichokishuhudia katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Manyema, lakini akasisitiza: "Hakuna mabadiliko ya ajabu yanayoweza kuonekana kesho, lakini tutajitahidi".
Simba ilitoka suluhu na Manyema katika mechi ya kwanza ambayo kocha huyo alikaa benchi akisaidiwa ma mzalendo,Jamhuri Kihwelo 'Julio' Jumatano.
Milovan alisema katika mechi yake ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika leo Jumapili dhidi ya Awassa City ya Ethiopia kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hatafanya mabadiliko ya kutisha na badala yake kazi kubwa ataifanya Julio.

No comments: