Wednesday, January 30, 2008
Lampard bado aendelea kusugua benchi Chelsea
Bado Arsenal Februari 17 Old Trafford
Sisi ndio yanga bwana..tunatisha
Dah! Kazi ngumu Man wanakimbia balaa...
Sasa sikilizieni makamuzi yangu
Tuesday, January 29, 2008
Twiga watagoma tena au?
Oya mshikaji Ulabu gani huo...?
Kakikohozi kwa sana na wese linashuka kichizi puani tangu juzi kati hapo,sijui ndio inakuwaje tena mambo kama hayo kwa mtu mzima kama hivi.Au huyu msela hapa kulia anafanya mambo fulani nini nimwachie liuwanja lakujinafasi?
Mambo yamekuwa mazito ikabidi watu wazima wamrudishe bwanamdogo bushi kidogo akaweke mambo sawa. Lakini sio ishu tujifanye hatujui.Basi juzi kati fulani bwana, mida ya jioni nikaibuka zangu mitaa yaUbalozi (jirani na hiyo klabu wanaita Lidaz) kule Kinondoni kwa nyumanyuma hivi sehemu fulani wanaita Octa Contena wanakoutwika wajanja.
Nilikuwa na mtu kama tatu zenye nyadhifa zao kwenye ofisi nzito nzito hukotawni ambao hata kuvusha wiki wakiutwika ‘twenti fo Awaz’ na kuegesha juuya meza kwao siyo ajabu.
Wakati watu wazima tunazidi kujinafasi na mamonde yaliyotanda zake mezani,kumbe bwana meza ya pili kuna masela fulani hivi kama wawili (nimetonywani Mapaparazi wenye maujiko ya kufa mtu Bongo hapa) mmoja kautwika zakemadude fulani hivi yanakaa kwenye maboksi(wanaita Penasoli sijui…kitu kamahicho) nafikiri kuanzia moningi jamaa anayagonga tu kwa mujibu wa wadau.
Kuna vagi kimtindo jamaa anakuja juu, hata macho hayataki tena kuona, basimwana mida hiyo masela huku pembeni burudaani… jamaa kazidiwa kanyanyukakwa msaada anaoujua mwenyewe kaibuka zake toileti.
Ni mida fulani ya saa mbili na ushee, masela zake wakangoja wee bila bilawakadhani labda jamaa kamwagiwa tindikali na Mafisadi au Jamaa fulaniwaliolamba mabilioni ya Biotii wamemzamisha toileti ili azibe mdomo,ikabidi wamuibukie.
Kumbe bwana msela maji yamezidi unga alipotoka zake kupunguza Toi,kasahau alipokuwa ameegesha kapapasa papasa geti la uani katokea Baa yajirani nako bado chaneli ikawa haikamati akaamua kutoka nje akaegeshakwenye lami ya Alhassan Mwinyi.
Duh! Blaza vipi tena?Mungu saidia Dada nanihii katafuta kichizi kila mahali kakosa,alipobahatisha Baa ya pili akaambiwa kuna msela alipita na ukuta hapamcheki labda rodini. Duh jamaa akanaswa bwana kaegesha rodinialiporejeshwa kwa masela wake anacheka mbavu hana…, nini kisa eti alijuayuko kwenye taxi anaenda Mwenge.
Duh! Blaza inakuaje ukinywa za uswahili?Uchune kidogo nikuambia ishu nyingine. Kiligi chetu cha Bongo ujuekinaanza leo kimtindo, wenye kupenda lahaa… tunaibuka zetu badayegraundini tukaangalie boli la wanetu siunajua tena tulikuwa tumelimisimida?
Lakini wana mmepiga matizi mwezi na ushee hatutaki kuona madudu na ushenziushenzi usiona na maana kama ilivyokuwa kwenye mzunguko ulijikata mwakajana ambao watu wazima Lunyasi na Jangwani walikiona cha moto kwa haowaliokuwa wakidhani ni mabwana wadogo.
Ubabe siyo ishu badilikeni wanangu, pigeni boli la akili kama tunalochekikwenye kideo huku Ghana, mangumi na kukanyagana kanyagana sio dili. Ndiomaana mnazidi kubanana Bongo tu na utajiri wa kutembelea Baluni na vyumbaviwili uswahilini.
Badilikeni mchezee mpira si miili ya watu, tumieni akili na vipaji vyakuzaliwa wazee sisi tunatoa mkwanja wetu hatuji kuuza sura tunakata kuonagemu tufurahi na magoli yafungwe si papara za ajabu zisizo na akili.Tulizeni akili msikilize mnachoambia na Maticha mtufanyie mambo, sisimkiendekeza ishu za ovyoovyo kama lasti raundi sisi tutakupigeni chini tukama vipi.
Tunakaa Baa tunapiga zetu ulabu na kuangalia kina Drogba, Eto’o na Kanuti. Haturembi simnajua zetu!Msiwe mizigo washikaji fungueni akili kuna ulaji kinoma Taifa Stars,muonyesheni mambo Maximo mle shavu na soka yetu ikue.
Ndio tunachotaka,ishu za ujiko ni baadae.
Ndio wakati wa kutuliza akili, kucheza na kuachana na mambo ya ajabu.Halafu kitu kipo laivu kwenye kideo cha Gitivii mjue! Ndio nafasi zenyeweza kujiuza nje hizo, onyesheni kujiamini mbona Kenya na Uganda wanaibukanje kibao na kufanya mambo kwani wenyewe wana miguu ya plastiki.
Acheni papara na anasa zisizo na msingi hiyo ni kazi wakubwa, tumieniutashi kuweni na ari ya mabadiliko tunakokwenda ni kugumu kichizi na umriunazidi kuyeyuka.Imefika enzi za wachezaji kubadilika na kuishi kama binadamu wa karnempya, msiridhike na maujiko ya uwanja wa Taifa mabega yakazidi vichwamkasahau kwamba kuna leo na kesho na maisha yako kama mchezaji yako miguu.
Kwamba mchezaji unaweza kuwa na mafanikio wakati ukiwa kwenye fomu keshona keshokutwa mambo yanaweza kubadilika. Na hivi wakazidi kuingia makochaWazungu patakuwa hapatoshi mkiendekeza uvivu na usupastaa wa kununuliwaKilimanjaro Uswahili mtaona Bongo chungu.Mtajichuja.
Na kwanini ifikie hatua hiyo? Wakati mna kila kitukinachostahili kwa nyie kibadilika na kufikia kwenye hatua inayokubalika.Oya washikaji pigeni kazi, embu jiskieni haya kidogo basi tupige na sisihatua kimataifa, kwanini mashabiki wenu wawe wawe wapweke kila sikukomaeni mtuinue Wabongo wenzenu wana.
Nasi tucheki wani dei. Mwanangu Songoro mitaa ya Chaga Baiti, Wili kwa Mapecos hapo na Wazee waNewvision, Sayansi kwenye kitimoto sana… tu! Leo Mtaumia, Mcameruni wenuatachomoka kwa Zambia iliyompiga Sudan tatu kwa mtungi?
Lwakatare naye ndani ya nyumba
Nyagawa alivyozamisha kitu langoni
Twiga Stars wana uelewa mdogo-TFF
Katibu Mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela alisema wachezaji hao kwa upeo wao walidhani shilingi milioni 2 zilizotolewa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete ni motisha yao kwa kuwafunga Eritrea.
"Uelewa wao mdogo ndio walitaka kugoma, walidhani zile hela zilizotolewa na Mama Kikwete ni zawadi yao walipoifunga Eritrea."alisema Mwakalebela ambaye ana kitambi.
"Zile fedha zilipoletwa nilimwambia meneja wao awalipe posho yao yote pamoja na walimu zilibaki laki moja nikamwambia ajaze yote mafuta basi la wachezaji linalowapeleka na kuwarudisha mazoezini.
"Mama Salma Kikwete alipotoa zile hela alisema ni za kuisaidia timu katika maandalizi yake dhidi ya Eritrea sasa wao kwa upeo wao sijui walivyoelewa wakahamasishana wakataka wapewe zile hela zote wagawane kama motisha wao wa Eritrea."
Aisha Madinda:Wameniambia niokoke nipone
“Wanasema kwamba endapo nikifanya kitu kama hicho naweza kupona haraka na kurejea kwenye hali yangu ya kawaida mapema kila mtu amekuwa akitoa maoni yake na nimekuwa nikiwaskiliza.
“Lakini bado sijaamua nini cha kufanya bado nataka kuzingatia matibabu ambayo nitakuwa napewa na madaktari wa Muhimbili kwanza halafu nione nini kitakachofuata lakini nina imani kwamba ipo siku hali yangu itakuwa vizuri,"Aisha alimwambia Mzee wa Kutibua jana jijini Dar es Salaam.
Hatari ya Athuman Iddi! Aisee..!
Shughuli iliyomleta ulimboka stars
Nataka Stars hii iwe juu sana
''Nimwachanganya kikosi changu kina wazoefu wachache na vijana wengi lakini nimefanya hivi ili hawa wenye uzoefu waweze kuwaongoza hawa vijana, lakini wanatakiwa kuonyesha uwezo wao uwanjani ili waweze kudumu kwenye kikosi cha Stars" alisema Maximo alivyotaja kikosi chake kipya jana kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi Februari 6.
Makipa -Ally Mustapha Simba , Farouk Ramadhan Shaaban Dihile JKT Ruvu.
Mabeki- Amir Maftah Nadil Haroub 'Cannovaro' (Yanga ) Said Swed (Simba) Meshack Abel, Salum Swed (Mtibwa) Salvatory Mtebe (Atraco) Erasto Nyoni (Vital o) Dennis Mukebezi (Coastal Union) na Stephano Mwasika (Prisons).
Viungo-Abdi Kassim, Athumani Idd, Castory Mumbala (Yanga) Ulimboka Mwakingwe Haruna Moshi na Henry Joseph (Simba) Shaaban Ndity na Kigi Makasi (Mtibwa Sugar) na Nizar Khalifan (Kuwait).
Washambuliji -Danny Mrwanda (Kuwait) Jerry Tegete na Vicent Barnabas, Yanga Athuman Machupa (Simba) na Uhuru Suleiman Coastal Union.