Wednesday, January 30, 2008

Lampard bado aendelea kusugua benchi Chelsea

Hali ya Kiungo wa Chelsea Frank Lampard bado haijatengamaa na huenda akakaa nje wiki mbili na atakosa mechi ya leo ya Ligi Kuu dhidi ya Readings kutokana na majeraha yanayomkabili. Mbali na mchezaji huyo hata Shevshenko na John Terry ni majeruhi.

Bado Arsenal Februari 17 Old Trafford


Man juzi ilipiga Spurs bao 3-1 kwenye michuano ya FA huyu bwana mdogo Ronaldo alipiga mawili na Terves akapiga bao la mwisho. Arsenal alimpiga Newcastle 3-0. Adebayor kapiga mbili jingine jamaa wamejifungua kimchecheto tu.

Sisi ndio yanga bwana..tunatisha


Yanga imefikisha pointi 24 katika msimamo wa Ligi sawa na Prisons inayoshikilia usukani. Lakini vijana hao wa jangwani wamedai kuitoa Prisons kileleni ni kazi ndogo na itaanza ijumaa hii dhidi ya Coast Union.

Dah! Kazi ngumu Man wanakimbia balaa...


Dah! kujikaza kote huko ndio kwanza pointi 39, nafasi ya sita Man U wana 54 yao kileleni tutawakamata kweli....! wasiwasi wangu wasije kumfukuza Benitez wangu tu.
Stephen Gerald-Liverpool.

Sasa sikilizieni makamuzi yangu


Ally Choki ambaye ameitosa Twanga Pepeta International na kuibukia zake TOT Plus ameibuka na kusema kuwa anakuja na madude manne mapya ya kufa mtu na kila mtu atabloo.

Choki ambaye sasa yupo zake mitaa ya Tabora kwenye ziara na bendi yake mpya amemhakikishia Mzee wa Kutibua ambaye ni mpenzi wa dansi kwamba muda si mrefu atavunja ukimya na kila mtu atashika mdomo.

Tuesday, January 29, 2008

Twiga watagoma tena au?


Shilingi mil. 7.5 zimetolewa na Benki ya Barclays kwa ajili ya kuisaidia Twiga Stars kwa maandalizi ya mchezo dhidi ya Cameroon wa utakaochezwa mwezi ujao kuwania tiketi ya kucheza fainali za Mataifa ya Afrika.

Wasiwasi wa Mzee wa Kutbua msije mkagoma tena mkifikiri ni za mgawo...!

Oya mshikaji Ulabu gani huo...?

ANGALAU! Lakini dah! Sijui itakuwaje masela, kuna ishu ishu fulani ambazondivyo sivyo kimtindo kwa mwanenu, inabidi tuteme mate chini tu.
Kakikohozi kwa sana na wese linashuka kichizi puani tangu juzi kati hapo,sijui ndio inakuwaje tena mambo kama hayo kwa mtu mzima kama hivi.Au huyu msela hapa kulia anafanya mambo fulani nini nimwachie liuwanja lakujinafasi?
Mambo yamekuwa mazito ikabidi watu wazima wamrudishe bwanamdogo bushi kidogo akaweke mambo sawa. Lakini sio ishu tujifanye hatujui.Basi juzi kati fulani bwana, mida ya jioni nikaibuka zangu mitaa yaUbalozi (jirani na hiyo klabu wanaita Lidaz) kule Kinondoni kwa nyumanyuma hivi sehemu fulani wanaita Octa Contena wanakoutwika wajanja.

Nilikuwa na mtu kama tatu zenye nyadhifa zao kwenye ofisi nzito nzito hukotawni ambao hata kuvusha wiki wakiutwika ‘twenti fo Awaz’ na kuegesha juuya meza kwao siyo ajabu.
Wakati watu wazima tunazidi kujinafasi na mamonde yaliyotanda zake mezani,kumbe bwana meza ya pili kuna masela fulani hivi kama wawili (nimetonywani Mapaparazi wenye maujiko ya kufa mtu Bongo hapa) mmoja kautwika zakemadude fulani hivi yanakaa kwenye maboksi(wanaita Penasoli sijui…kitu kamahicho) nafikiri kuanzia moningi jamaa anayagonga tu kwa mujibu wa wadau.
Kuna vagi kimtindo jamaa anakuja juu, hata macho hayataki tena kuona, basimwana mida hiyo masela huku pembeni burudaani… jamaa kazidiwa kanyanyukakwa msaada anaoujua mwenyewe kaibuka zake toileti.
Ni mida fulani ya saa mbili na ushee, masela zake wakangoja wee bila bilawakadhani labda jamaa kamwagiwa tindikali na Mafisadi au Jamaa fulaniwaliolamba mabilioni ya Biotii wamemzamisha toileti ili azibe mdomo,ikabidi wamuibukie.
Kumbe bwana msela maji yamezidi unga alipotoka zake kupunguza Toi,kasahau alipokuwa ameegesha kapapasa papasa geti la uani katokea Baa yajirani nako bado chaneli ikawa haikamati akaamua kutoka nje akaegeshakwenye lami ya Alhassan Mwinyi.
Duh! Blaza vipi tena?Mungu saidia Dada nanihii katafuta kichizi kila mahali kakosa,alipobahatisha Baa ya pili akaambiwa kuna msela alipita na ukuta hapamcheki labda rodini. Duh jamaa akanaswa bwana kaegesha rodinialiporejeshwa kwa masela wake anacheka mbavu hana…, nini kisa eti alijuayuko kwenye taxi anaenda Mwenge.
Duh! Blaza inakuaje ukinywa za uswahili?Uchune kidogo nikuambia ishu nyingine. Kiligi chetu cha Bongo ujuekinaanza leo kimtindo, wenye kupenda lahaa… tunaibuka zetu badayegraundini tukaangalie boli la wanetu siunajua tena tulikuwa tumelimisimida?
Lakini wana mmepiga matizi mwezi na ushee hatutaki kuona madudu na ushenziushenzi usiona na maana kama ilivyokuwa kwenye mzunguko ulijikata mwakajana ambao watu wazima Lunyasi na Jangwani walikiona cha moto kwa haowaliokuwa wakidhani ni mabwana wadogo.
Ubabe siyo ishu badilikeni wanangu, pigeni boli la akili kama tunalochekikwenye kideo huku Ghana, mangumi na kukanyagana kanyagana sio dili. Ndiomaana mnazidi kubanana Bongo tu na utajiri wa kutembelea Baluni na vyumbaviwili uswahilini.
Badilikeni mchezee mpira si miili ya watu, tumieni akili na vipaji vyakuzaliwa wazee sisi tunatoa mkwanja wetu hatuji kuuza sura tunakata kuonagemu tufurahi na magoli yafungwe si papara za ajabu zisizo na akili.Tulizeni akili msikilize mnachoambia na Maticha mtufanyie mambo, sisimkiendekeza ishu za ovyoovyo kama lasti raundi sisi tutakupigeni chini tukama vipi.
Tunakaa Baa tunapiga zetu ulabu na kuangalia kina Drogba, Eto’o na Kanuti. Haturembi simnajua zetu!Msiwe mizigo washikaji fungueni akili kuna ulaji kinoma Taifa Stars,muonyesheni mambo Maximo mle shavu na soka yetu ikue.
Ndio tunachotaka,ishu za ujiko ni baadae.
Ndio wakati wa kutuliza akili, kucheza na kuachana na mambo ya ajabu.Halafu kitu kipo laivu kwenye kideo cha Gitivii mjue! Ndio nafasi zenyeweza kujiuza nje hizo, onyesheni kujiamini mbona Kenya na Uganda wanaibukanje kibao na kufanya mambo kwani wenyewe wana miguu ya plastiki.
Acheni papara na anasa zisizo na msingi hiyo ni kazi wakubwa, tumieniutashi kuweni na ari ya mabadiliko tunakokwenda ni kugumu kichizi na umriunazidi kuyeyuka.Imefika enzi za wachezaji kubadilika na kuishi kama binadamu wa karnempya, msiridhike na maujiko ya uwanja wa Taifa mabega yakazidi vichwamkasahau kwamba kuna leo na kesho na maisha yako kama mchezaji yako miguu.
Kwamba mchezaji unaweza kuwa na mafanikio wakati ukiwa kwenye fomu keshona keshokutwa mambo yanaweza kubadilika. Na hivi wakazidi kuingia makochaWazungu patakuwa hapatoshi mkiendekeza uvivu na usupastaa wa kununuliwaKilimanjaro Uswahili mtaona Bongo chungu.Mtajichuja.
Na kwanini ifikie hatua hiyo? Wakati mna kila kitukinachostahili kwa nyie kibadilika na kufikia kwenye hatua inayokubalika.Oya washikaji pigeni kazi, embu jiskieni haya kidogo basi tupige na sisihatua kimataifa, kwanini mashabiki wenu wawe wawe wapweke kila sikukomaeni mtuinue Wabongo wenzenu wana.
Nasi tucheki wani dei. Mwanangu Songoro mitaa ya Chaga Baiti, Wili kwa Mapecos hapo na Wazee waNewvision, Sayansi kwenye kitimoto sana… tu! Leo Mtaumia, Mcameruni wenuatachomoka kwa Zambia iliyompiga Sudan tatu kwa mtungi?

Hawa ndio cameroon bwana!


Lwakatare naye ndani ya nyumba


Mbunge wa viti maalum, mchungaji Getrude Lwakatare akila kiapo jana Bungeni mjini Dodoma. Ameziba nafasi ya Salome Mbatia aliyefariki hivikaribuni kwa ajali ya gari.

Hawa ni Simba Wako Coco Bichi bwana wanajifua!


Nyagawa alivyozamisha kitu langoni


Kiungo mshambuliaji wa Simba Nico Nyagawa alipomtoka, kipa wa Coast Union Ismail Suma na kupiga kitu nyavuni na kuandika bao la kwanza kwa wekundu wa Msimbazi hapo Taifa. Simba ilishinda 2-1.

Twiga Stars wana uelewa mdogo-TFF


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema uelewa mdogo wa wachezaji ndio uliosababisha kutishia kugomea kambi ya timu hiyo iliyopo kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela alisema wachezaji hao kwa upeo wao walidhani shilingi milioni 2 zilizotolewa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete ni motisha yao kwa kuwafunga Eritrea.
"Uelewa wao mdogo ndio walitaka kugoma, walidhani zile hela zilizotolewa na Mama Kikwete ni zawadi yao walipoifunga Eritrea."alisema Mwakalebela ambaye ana kitambi.
"Zile fedha zilipoletwa nilimwambia meneja wao awalipe posho yao yote pamoja na walimu zilibaki laki moja nikamwambia ajaze yote mafuta basi la wachezaji linalowapeleka na kuwarudisha mazoezini.
"Mama Salma Kikwete alipotoa zile hela alisema ni za kuisaidia timu katika maandalizi yake dhidi ya Eritrea sasa wao kwa upeo wao sijui walivyoelewa wakahamasishana wakataka wapewe zile hela zote wagawane kama motisha wao wa Eritrea."

Aisha Madinda:Wameniambia niokoke nipone


“Nimepokea simu kwa mamia na meseji nyingi sana, ila kuna wasamaria wamekuwa wakinishauri mara kwa mara kwamba niokoke na kumrejea Mungu kutokana na hali niliyonayo.
“Wanasema kwamba endapo nikifanya kitu kama hicho naweza kupona haraka na kurejea kwenye hali yangu ya kawaida mapema kila mtu amekuwa akitoa maoni yake na nimekuwa nikiwaskiliza.
“Lakini bado sijaamua nini cha kufanya bado nataka kuzingatia matibabu ambayo nitakuwa napewa na madaktari wa Muhimbili kwanza halafu nione nini kitakachofuata lakini nina imani kwamba ipo siku hali yangu itakuwa vizuri,"Aisha alimwambia Mzee wa Kutibua jana jijini Dar es Salaam.

Mwanamama huyo mwenye watoto wawili wanaosoma sekondari amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya moyo kujaa maji na miguu yake sasa imevimba kiasi kwamba anashinda hata kuvaa viatu wala hajaenda kwenye maonyesho kama miezi mitatu sasa imepita. Baaadhi ya wanyetishaji wasio na dogo wamekuwa wakiihusisha hali yake na imani za kishirikina.

Hatari ya Athuman Iddi! Aisee..!


Athuman Iddi wa Yanga alipogongana na mchezaji wa Ashanti na kuumia vibaya kwenye mechi ya kwanza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Bara. Hakukuwa na watu wa huduma ya kwanza kwenye uwanja wa Taifa siku hiyo na ililazimika mchezaji wa Ashanti kukimbizwa hospitali kwa gari binafsi ya shabiki mmoja. TFF why....kwaniniiiiiiii?

Shughuli iliyomleta ulimboka stars


"Hii najipinda halafu naizungusha, nachomoka hivi, mi ndio ulimboka bwana ukisikia mwingine ni photocopy."
Jamaa anasemaje unajua: Nimefurahi sana, huu ndio wakati wangu wa kuonyesha mambo adimu .

Nataka Stars hii iwe juu sana




''Nimwachanganya kikosi changu kina wazoefu wachache na vijana wengi lakini nimefanya hivi ili hawa wenye uzoefu waweze kuwaongoza hawa vijana, lakini wanatakiwa kuonyesha uwezo wao uwanjani ili waweze kudumu kwenye kikosi cha Stars" alisema Maximo alivyotaja kikosi chake kipya jana kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi Februari 6.
Makipa -Ally Mustapha Simba , Farouk Ramadhan Shaaban Dihile JKT Ruvu.
Mabeki- Amir Maftah Nadil Haroub 'Cannovaro' (Yanga ) Said Swed (Simba) Meshack Abel, Salum Swed (Mtibwa) Salvatory Mtebe (Atraco) Erasto Nyoni (Vital o) Dennis Mukebezi (Coastal Union) na Stephano Mwasika (Prisons).
Viungo-Abdi Kassim, Athumani Idd, Castory Mumbala (Yanga) Ulimboka Mwakingwe Haruna Moshi na Henry Joseph (Simba) Shaaban Ndity na Kigi Makasi (Mtibwa Sugar) na Nizar Khalifan (Kuwait).
Washambuliji -Danny Mrwanda (Kuwait) Jerry Tegete na Vicent Barnabas, Yanga Athuman Machupa (Simba) na Uhuru Suleiman Coastal Union.