Friday, February 22, 2008

Huu wa Arsenal Wenga ni ukoloni


EBWANA wanangu inakuwaje? Ishu zinaendaje mitaa ya kati hapo, shukrani sana kwa kukodolea macho mitaa hii linakomwaga sera Zee la Kutibua.
Mwanenu lasti wiki ishu zilikuwa nuksi kichizi, mijicho ilikuwa haitaki kuona mambo fulani.
Jamaa zangu fulani ambao hawajaaga Mpwapwa kama Mzee wa Sumo wanaweza kufungasha virago wakidhani ni pua ya mtaalam inafanya mambo yake.
Unafanya mchezo nini? Yaani Red aiyizi noma nakwambia, hata wakaanga sumu macho yao yana nafuu.
Lakini shwari kimtindo Mzee mzima sasa niko freshi napeta zangu kwenye viunga vya Kandoro ambavyo porojo za kifisadi zimepotea kijiweni na kilichobaki ni simulizi mpaka za buti za Bush.
Si baaada ya Bush kutua na midege yake? Palikuwa hapatoshi wana! Hata wauza mihogo wa mtaani kwetu Vingunguti Kiembe Mbuzi walipiga zao mguu na kuibuka Eapoti kumshangaa mshkaji.
Waliobaki uswahili na wenyewe ni vimbwanga tupu, muda wote mijicho haibanduki angani wakishuhudia mihemko na mbwembwe za midege ‘Eafosi wani’.
Wapo wadeni waliobonyeza Mzee wa Kutibua na kumtonya kwamba ujio wa mshkaji umewasevu pia na kuwapa mwanya wa kupishana milangoni kwani wenye mapango walinogewa na soga na kuhamishia bongo zao skani.
Lakini tukiacha porojo hili la FA kutaka kutulelea ligi yao bongo silikubali. Haiwezekani huku ni kutumaliza kabisa pamoja na kidogo tulichonacho.
Wiki chache zilizopita kamati ya Ligi Kuu ya England ilitoa pendekezo na kuonyesha nia ya kutaka Ligi Kuu ya nchi hiyo baadhi ya mechi zake zichezwe kwenye nchi nyingine Duniani ifikapo msimu wa 2010-11.
Rais wa FIFA, Sepp Blatter ameibuka na kupinga mapendekezo hayo kwa kile alichoeleza kwamba ni kinyume na sheria na kwamba itakuwa ni kuangamiza ligi za nchi nyingine.
Jamaa akaendelea kueleza kwamba itatibua pia kampeni za Weldi kapu 2018. Lakini baada yake Aseno Wenga ambaye ni kocha wa Aseno akaibukia kusikojulikana madai yake ni kwamba Blata kachemka.
Anachosema Wenga ni kwamba ligi iruhusiwe kuchezwa nje ili kutangaza zaidi ligi yenye ushindani, kutoa nafasi kwa mashabiki kufaidi uhondo ikiwemo pia kwa klabu husika kujiingiza mamilioni. Mzee Wenga pamoja na Uprofesa wako na hao jamaa wa FA hatutaki.
Lakini wana hii ishu mi sikubaliani nayo! Tukiwaruhusu wakicheza tu Afrika tumekwisha na ndio mwanzo wa kuuwa kabisa ligi na klabu zetu. FA inataka mechi moja ya mwisho kila msimu kwa kila timu ihamishiwe Afrika, Asia au Amerika.
Kwa hali ilivyo sasa mashabiki asilimia kubwa wanabeza ligi zao za nyumbani na kushabikia klabu za England ambazo wanaziona kwenye kideo. Je zikija kucheza hizo mechi zao moja moja Afrika au kwenye hizo nchini nyingine si ndio watatuuwa kabisa na msisimko wote wa mashabiki utahamia Ulaya na kupuuza ligi zao na wachezaji wao?
Hakuna siri kwamba ligi hata klabu nyingi za Afrika bado ni changa na zinahitaji sapoti kubwa ili kuzipandisha katika kiwango ambacho angalau kitakaribiana na wenzetu walioendelea lakini kwa kuwakaribisha wenzetu watumie ardhi yetu ni kupotea maboya.
Tunapaswa kulinda klabu zetu na ligi zetu sasa, Waingereza wametutawala mno kwa kila kitu haiwezekani watuletee mpaka na ligi yao kana kwamba sisi hatuna thamani. Mbona wao hawasemi zetu zikachezwe kwao?
Najua kwa mashabiki ‘walevi’ wa kina Ronaldo wa Machesta, Fabregas wa Aseno au Lampard wa Chelsii hata Gerad wa Livapulu watafurahia wazo la ligi hiyo kuchezwa nje na kuongezwa hadi 39 badala 38 ili wawaone wachezaji wao lakini hasara zake ni nyingi kuliko faida.
Nani atahangaika na Masumbuko wa Mtibwa,Ulimboka wa Simba,Tegete wa Yanga au Mangunguru wa Moro?
Kama lengo lao ni kuja kucheza na klabu zetu kuzipa uzoefu na kubadilishana baadhi ya mambo sawa, lakini si mje mkacheze wenyewe kwa wenyewe.Hakuna faida kwa hilo kwa nchi kama Tanzania zaidi ya kuuwa kabisa ligi yetu. Waingereza wametuletea teknolojia nyingi za kisasa, wametulazimisha kuiga mfumo wao wa maisha tukaachana hata mambo yetu ya kiutamaduni kwa madai kuwa tunakwenda na wakati sasa wamekaa wamefikiria na ligi zetu za ndani hazina maana wameona watuletea zao? Kwanini tukandamizwe kiivyo, lazima tujifunze kuwa maskini jeuri?
Tusikubali kushikwa masikio kwa kila kitu anachoamua mzungu hata kama ni cha kipuuzi, kwa nini ligi yao wasicheze huko huko kwao?
Muda wa kutawaliwa kifikra umekwisha, walishatukalia miaka ya nyuma na kutuweka mifuko mwao, tukajitahidi tukapata uhuru wetu tusiwakaribishe tena watutawale watatuharibia timu zetu za Taifa.
Si wacheze kwenye viwanja vyao sisi tutawaangalia kwenye kideo kwani lazima waje Afrika? Labda Asia na mabara mengine.
Ni changamoto sasa kuwekeza na kuhakikisha ligi zetu zinapiga hatua kwenda kwenye kulipwa waliko wenzetu na tujitahidi kujifunza zaidi kila kunapokucha na tusikubali kuendeshwa na wakubwa kana kwamba sisi hatuna akili wala ujuzi wa kupanga mambo yetu, huu ni ukoloni wa waziwazi.
Mzee wa Kutibua anatia zake nanga mitaa hii, lakini wana..tuibukeni Taifa tukawapige tafu dada zetu wa Twiga Stars, wanatisha kinoma si umeskia leo wanakipiga na mademu wa Kameruni? Tuibuke halafu badaye kama kawa Mugongo...Mugongo..!
Wengine Samaki ana vipande vingapi..!
0713374649
HYPERLINK mailto:momburi2002@yahoo.com
Mzeewakutibua.blogspot.com

Thursday, February 21, 2008

Kikosi cha Mizinga chaanza kutisha


Kundi la Kikosi cha Mizinga cha Jijini Dar es Salaam limeanza kampeni ya kupambana na madawa ya kulevya kwa wasanii wa muziki huo kupitia maonyesho maalum yatakayofanyika kwenye ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu Kalapina ambaye ni kiongozi wa kundi hilo shoo ya kwanza itafanyika keshokutwa jumapili na wasanii kibao akiwemo Rado watawapiga tafu.

Kikwete- Twiga Stars mnaweza komaeni

RAIS Jakaya Kikwete amewataka wachezaji wa timu yasoka ya wanawake Twiga Stars kucheza kwa kujiaminiwatakapopambana na Cameroon Jumamosi, akisema "mnavyoonekana mnaweza"
Rais Kikwete amesema hayo jana Ikulu jijini Dar Es Salaam wakati wa chakula cha usiku alichowaandalia wachezaji wa Twiga Stars kwa ajili ya kufahamiana kwa kuwa hakupata fursa ya kuwatembelea kambini.
Twiga Stars itapambana na Cameroon katika michuano yaawali ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za Mataifa ya Afrika baada ya kuwatoa Eritrea kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2.Fainali za michuano hiyo zinatarajiwa kufanyika Guinea Juni mwaka huu.
Rais alisema: “Mnacheza na Cameroon yenye jina kubwa katika soka la wanaume si wanawake. Hakutakuwepo na Eto’o.
Mtoke hapa muingie kiwanjani mkiamini niko nanyi. Jiaminini na mjue kuwa nyinyi ndio mtakaoshinda na Watanzania wote wako nyuma yenu. Soka la wanawake halina muda mrefu kinachotakiwa ni kujiamini na kuungwa mkono.”

Hii ya Simba ni hatari kubwa


Timu ya Simba imelazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar na kufikisha pointi 24 ambazo ni hatari kwake kwani katika mechi iliyopita ilitoa suluhu na Manyema United inayokaribia kushuka daraja.

Endapo Simba isipojirekebisha huenda ikampaka faida mtani wake Yanga mwenye pointi 33 ambaye akishinda mechi sita tu kuanzia sasa anamvua ubingwa kwa kufikisha pointi 51 kwani Simba ikishinda zote nane ilizonazo kwa sasa itafikisha pointi 48 tu na kuinua mikono juu. Machupa, Ulimboka mpo?

Aisee.. sijapata kuona hii


Rais Jakaya Kikwete,Makamu wa Rais, Mohamed Shein na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakishangaa jambo wakati walipokuwa kwenye uwanja wa ndege juzi wakimuaga Rais Bush aliyekuwa na ziara ya siku nne hapa nchini.

Sunday, February 17, 2008

Shevchenko arudi AC Milan


AC Milan wanataka kumrejesha Italia mshambuliaji wa Chelsea Andry Shevchenko kwa madai kuwa amekuwa akiwasiliana nao mara kwa mara na wanaamini bado nafasi yake ipo kwenye kikosi hicho.

Simba Full kujiachia, Yanga heee...!


Simba jana ilianza mambo kwenye Ligi ya mabingwa baada ya kuipiga Awassa ya Ethiopia mabao 3-0 kwenye uwanja wa Taifa. Moses Odhiambo kapiga mbili na Ulimboka Mwakigwe moja.

Yanga iliyokuwa Madagascar ikikipiga na As Adema, ilifungwa 1-0 huku ikicheza kwenye mvua kubwa.

Makocha wa Yanga wampa Umbea Milovan


MAKOCHA wa Yanga, Kondic Dusan na Spaso Solokovisk (kwenye picha) wamemweka kitako na kumueleza kila kitu kocha mpya wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic.

Milovan alitua nchini wiki iliyopita alisaini mkataba wa mwaka mmoja na Wekundu hao kwa mujibu wa Mwenyekiti wa klabu hiyo, Hassan Dalali. Katika mechi ya Ligi Kuu ya Bara, baina ya Prisons na Manyema juzi kwenye uwanja wa Taifa, Kondic, Spaso na kocha wa vijana wa Yanga, Zivojnov Srdan walimchukua kocha Milovan na kukaa nae zaidi ya dakika 25. Prisons ilishinda 4-1.

Hali hiyo ambayo iliwashangaza baadhi ya viongozi wa klabu hizo ambao ilibidi waduwae kwa vile si jambo la kawaida katika miaka ya hivikaribuni kwa makocha wa timu hizo hasimu kukaa na kubadilishana mawazo kwa muda mrefu.Tukio hilo ambalo lilitokea kwenye jukwaa la wageni wa heshima (VIP) wakati wa mapumziko ya mchezo huo lilitokana na makocha hao wenye hadhi ya Uprofesa kufahamiana kiundani kwa miaka mingi tangu wakiwa kwao Serbia.

Miembeni,Chipukizi mdebwedo kabisa


KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Afrika Kusini na klabu ya Simba, Trott Moloto ametua nchini akiwa na kikosi cha Mamelodi Sundowns ambayo imeifunga Miembeni ya Zanzibar(pichani) 1-0 katika mechi ya awali ya Ligi ya Mabingwa kwenye uwanja wa Amaan jana jumamosi.

Kwenye kombe la Shirikisho Bufallo ya Zambia imeifunga Chipukizi ya Pemba mabao 5-0. This is too much aiseee 5-0? Ndio kwisha kazi tena.

Huendi mahali sisi ndio Ashanti Utd


"Sisi ndio watoto wa Jiji bwana, mwaka jana simlisema hivyo hivyo tutashuka sisi hatushuki daraja tunazidi kupeta tu mwendo ule ule na wachezaji tutauza kama kawa,"alisema Msafiri Mgoyi ambaye ni rais wa Ashanti United alipozungumza na waandishi wa Blog hii.

Ashanti ina pointi 18 tu na ni miongoni mwa timu nne zinazopewa nafasi kubwa ya kushuka daraja. Nyingine ni Polisi Dodoma, Manyema na Pan Africa ya Kariakoo.


Julio azikunja na Mashabiki Taifa


Kitendo cha mashabiki wa Simba, kumtukana kocha wao msaidizi Jamhuri Kihwelu 'Julio' kilimkera bosi huyo na kuamua kuzikunja baada ya kumalizika kwa mechi dhidi ya mechi wiki iliyopita ambayo matokeo yake yalikuwa suluhu.

Julio(anayetoa lekcha hapo) aliwachenjia mashabiki huku akissisitiza " Najiuzulu nakuachieni timu yenu, hamuwezi kuniletea mambo ya kipuuzi nitakuachieni huyo mzungu wenu...haiwezekani najiuzulu nasema"

Ujasiri wa kufumba macho


LICHA ya kukosa mechi za kimataifa za kujipima nguvu, Kocha mkuu wa timu ya soka ya taifa ya wanawake 'Twiga Stars' Charles Boniface amesema kikosi chake kina mabadiliko makubwa kiuchezaji.
"Naona sasa kuna mabadiliko kiuchezaji lakini kikubwa ni kuanza kujiamini, wachezaji sasa wanajiamini kutokana na kuondoa woga ni mambo madogo tu ya kitoto bado tunajaribu kuyaondoa," alisema Mkwasa.

Lakini licha ya matizi ya kufa mtu yanayopigwa na hawa vijana kwenye uwanja wa Karume bado wataalam wa mambo wanadai ni ngumu kuifunga Cameroon kwa kucheza na timu za Uswazi na wazee wanaotokea Bar kwenye mazoezini.

Hichi kijamaa ni noma-Neville


LONDON, England

BEKI na nahodha wa Manchester United, Gary Neville amewatahadhalisha wapinzani wao wa Kombe la FA timu ya Arsenal kuwa waaangalifu na Cristiano Ronaldo(pichani) kwa sababu anacheza soka ya sayari nyingine msimu huu.
Nahodha huyo Neville ambaye amekuwa benchi kwa muda mrefu msimu kutokana na kuwa majeruhi, amesisitiza Ronaldo sasa ni sawa na nyota wengine wa Red Devils, kama Eric Cantona, Roy Keane na David Beckham.
Neville, 32, alisema: “Katika suala kuburudisha, kutegeneza na kufunga, utapenda kumuona mchezaji huyu akiwa na mpira. Ni mchezaji wa kutoka sayari nyingine.”

Ronaldo kwisha kazi yake


PARIS, Ufaransa

MSHAMBULIAJI Ronaldo de Lima ameendelea kuandamwa na jinamizi la kuwa majeruhi akiwa na AC Milan baadaye kumia mguu na kufanyiwa operesheni itayomweka nje ya uwanja kwa miezi tisa.

Ronaldo alifanyiwa upasuaji huo katika hospitali ya Pieté-Salpetriere mjini Paris ilo fanyika kwa usalama juzi usiku kwa mujibu magezeti ya Ufaransa. Operesheni hiyo ilifanyika saa 3:00 usiku chini ya Professor, Gerrard Saillant ambaye alimfanyia Ronaldo upasuaji wa goti lake la mguu wa kushoto. Baada ya upasuaji huo daktari huyo alielezea jinsi hali ilivyokuwa ya mafanikio.

Fabregas haondoki tena milele


LONDON, Englan

KIUNGO Cesc Fabregas ameingia mkataba mnono wa pauni milioni 33 (Sh bilioni 75) utakaomfanya kuwa moja ya mchezaji anayelipwa zaidi katika historia ya klabu ya Arsenal. Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amemtaka kiungo huyo wa Hispania ajitie kitanzi cha kuichezea klabu hiyo hadi 2016 kwa kuongeza miaka miwili katika mkataba wake wa sasa. Fabregas ambaye alikuwa akilipwa pauni 50,000 kwa wiki sasa atalipwa pauni 80,000 kwa wiki. (Pauni 80,000 ni sawa na Sh milioni 180)

Kanye West afunika Grammy

MWANAMUZIKI wa Uingereza, Amy Winehouse na mzoefu Kanye West ndio waliofunika tamasha kubwa duniani la kutuza wanamuziki la Grammy ambalo lilifanyika Jumapili iliyopita ikiwa ni mara ya 50 tangu kuanzishwa.Lakini wanamuziki hao wawili waliikosa tuzo kubwa ya Albamu Bora ya Mwaka iliyonyakuliwa na Herbie Hancock inayoitwa "River: The Joni Letters", ambayo ni mkusanyiko wa nyimbo za mkali wa nyimbo za jazz, Joni Mitchell (ikiwa na wasanii waalikwa ambao ni wapiga gitaa maarufu kama Norah Jones, Tina Turner, na Corrine Bailey Rae).Winehouse, ambaye alitumbuiza kibao chake cha ''I'm No Good'' na ''Rehab'' kupitia luninga akiwa jijini London, nusura atwae tuzo zote alizotajwa kuwania.

Saturday, February 16, 2008

Anelka aibeza Arsenal


Nicolas Anelka amesema: Sisi hatuogopi maneno ya watu, bado Chelsea ina nafasi ya kusonga mbele na kutwaa ubingwa wa England na makombe mengine yote tunayowania."

"Hatuna wasiwasi na upinzani uliopo, sisi jukumu letu ni kushinda na kuwafurahisha mashabiki,"alisema Anelka jana.

Anelka alijiunga na Chelsea hivikaribuni akitokea Bolton.

Arsenal this is too much wazee..!


Licha ya kuwa kinara kwenye Ligi Kuu ya England, Arsenal jana ilichakazwa bao 4-0 na Manchester United kwenye mechi ya kombe la FA. Darren Fletcher kapiga mbili, Nani na Rooney wakamaliza kazi.

Milovan ampa shavu Julio


KOCHA mpya wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic amekiri kuwa ana kazi kubwa ya kuibadili timu hiyo kutokana na kiwango alichokishuhudia katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Manyema, lakini akasisitiza: "Hakuna mabadiliko ya ajabu yanayoweza kuonekana kesho, lakini tutajitahidi".
Simba ilitoka suluhu na Manyema katika mechi ya kwanza ambayo kocha huyo alikaa benchi akisaidiwa ma mzalendo,Jamhuri Kihwelo 'Julio' Jumatano.
Milovan alisema katika mechi yake ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika leo Jumapili dhidi ya Awassa City ya Ethiopia kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hatafanya mabadiliko ya kutisha na badala yake kazi kubwa ataifanya Julio.

Simba, Yanga zipo kazini


ZIKIWA chini ya maprofesa kutoka Serbia, Simba na Yanga zinaanza rasmi kazi nyeti za kimataifa zitakapokuwa katika viwanja tofauti kesho Jumapili.
Yanga chini ya Profesa, Kondic Dusan na msaidizi wake Spaso Solokovisk ipo mjini Antananarivo, Madagascar kuivaa AS Adema ya huko kwenye mechi ya raundi ya awali ya Kombe la Shirikisho.

Simba ya Mtaalam Milovan Cirkovic ipo kwenye uwanja wa Taifa ikiivaa Awassa ya Ethiopia.

Atanyongwa mtu nakwambieni...

MASELA wengine nuksi tu, aheri hata wangebadilishwa na Magunia ya mkaa tukajua moja tu.Bora tu kwani ni nini bwana? Tena laifu ingesonga tu kiulaini kinoma.
Tunawekeana viwingu viwingu vya kizushi bwana laifu lenyewe lipi bwana kibongo bongo na mwendo wetu wa Daladala.
Longolongo nyingi halafu wanatutibulia ishu zetu tu, utafikiri virusi bwana! Kila ukitulia kwenye engo yako unakula zako ‘Uwele’ na wajisiriamali mkipanga mishemishe za hapa na pale wamo, wameibuka na vijimambo vyao, inakuwaje kiivyo wana? Au kuweka maskani ya muda Shamba imekuwa nongwa?
Mara oooh..Mzee mzima hongera bwana nimeona jana waifu katuletea kitu kipya mtaani bwana...
Bado jamaa zinaendelea tu, nkafikiri labda shida ni kilauri nikawachapa moja moja ili wasepe na ishu zao. Bwana si wakazidi kumwaga umbea bwana...? Mara oooh... nimeskia jamaa unamuoa tena nanihii bwana inakuwaje mbona hivyo...!
Si wakazidi kuniganda bwana...mpaka wakaniachia Redi Aizi rafiki yangu. Naiti naibuka homu mambo si yakaanza kujibu yaani noma tupu, mzee mzima nimeumbuka mchana kweupee.. jicho halifai. Au kuna pua ya mtu nini Masela?
Waliomshtukia Mzee wa Kutibua akinyatanyata kwenye korido za tabibu fulani mitaa ya Kinondoni wakamuibukia na kumshauri eti anawie mkojo wa mademu ishu itakata fasta. Eh! Si wana watanikimbia Bongo? Haiwezekani hiyo wakubwa.
Lakini ishu zinasonga ingawa mambo si mambo kwenye waleti za wanangu fulani ambao kupiga mguu siku kama hizi kukatiza mitaa ya Kino kuibukia Dasilamu mjini ni ishu ya kawaida.
Ndio maisha ya bongo hayo, usione jamaa linamwagika jasho ukafikiri ni misosi imekubali. Mambo yametaiti kila kona, nani arudi Itigi aiache Samora Avenyuu Darisalamu. Unacheza... nini!
Ebu ngoja kwanza nkupe ishu! Hawa wababaishaji wanaojifanya wanazipenda timu zao wakiendelea kuendekezwa kwenye uwanja wa Taifa, iko siku watanyonga mtu na mtalia.
Tiefuefu na Polisi fungueni macho, Musiwe wanafiki hivi vitendo vinavyofanywa na mashabiki wa Pan Africa na majirani zao wa Ashanti ni hatari kwa maisha ya binadamu.
Tumekuwa tukishuhudia katika mechi zinazohusisha timu hizo mashabiki wenye jazba wakisogelea mabenchi yao ya ufundi mara kadhaa na kutukana na kutishia makocha na wachezaji.
Baadhi wamekuwa wakikera wachezaji na kuwapotezea umakini wa kusoma na kuangalia kwa kusimama kwenye uzito karibu na mabenchi na kuwatishia.
Lakini cha kusikitisha zaidi tumeshuhudia wengine wakipenya uzio kwa kupitia kwenye geti kubwa kwenda mpaka kwenye benchi kutishia kwa maneno makocha huku wakiwaelekeza kufanya mabadiliko? Nini kazi ya hao Polisi getini?
Vitendo hivyo ambavyo vya kibabaishaji, vinavyofanywa na baadhi ya mashabiki ambao sisiti kusema ni wababaisha ni vya kudhalilisha taaluma kwa makocha husika na kuvuruga wachezaji.
Napata ugumu kuelewa upeo na wanachofikiria viongozi wa klabu hizo ambao kwa mara kadhaa tangu vitendo hivyo vimekuwa vikionekana kwenye uwanja wa Taifa sikupata kusikia au kuona wakitamka chochote. Msafiri vipi bwana! Au ndio kawaida Ki-Ilala Ilala?
Haiwezekani shabiki tena Mzee wa miaka isiyopungua 60 anatoka jukwaani huku akishangilia na wanazi wengine anapenya uzio ulio chini ya Polisi na kwenda kuwafokea makocha kwenye benchi huku ngazi zinazohusika kila mmoja akishuhudia.
Akienda na silaha akamchoma kocha au mchezaji je?Nani atawajibika kwenye hili na ni uzembe wa nani?
Kwanini kila mtu asipewe nafasi na kutekeleza majukumu yake kiufasaha? Hawa wababaishaji wataendekezwa mpaka lini. Kwanza wana mchango gani kwa klabu zaidi ya kujitokeza tu na kuanza kupiga makelele uwanjani, unazi gani huo wa kishamba wakubwa?
Viongozi wa hizi klabu za Ashanti na Pan Africa wanapaswa kuwaelemisha na kuwadhibiti mashabiki wao. Hata Tiefuefu inapaswa kushikilia makali zaidi kwa kuhakikisha kila mtu anakuwa huru kutekeleza majukumu yake na wababaishaji wanaojifanya wana machungu wadhibitiwe na sifa za kijinga ziwaishe.
Haiwezekani watu wenye ‘mamulhaka’ tukalea vikundi vya mashabiki wachache wanaotaka kutuvuruga na kutupotezea uelekeo. Hawana jipya na naamini hata fomesheni pengine hawajui kabisa. Kwanini tunalea uozo kama huu?
Ebwana wanangu eee... naingia mitini kimtindo. Mwanangu Uli, Machupa ...ee..kesho vipi Taifa hapo? Mshkaji wangu Ben, Ngassa...ee inakuwaje Madagasca hapo itakuwaje?
Sasa ni intaneshno mechez kuanzia kesho. Simnajua? Tuache unazi wa kishamba, tuweke mbele uzalendo tushangilie Wanaume wasonge mbele.
Utani sio uadui... achaneni na ushabiki wa mwaka Arobaini na saba mbona mabosi wenu wanakaa meza moja hamuoni hata hao wazungu wanapiga kinywaji pamoja?
Bofya basi kwenye MZEEWAKUTIBUA.BLOGSPOT.COM utaliona laivu zee la Kutibua. Badae kama kawa Kungwasumika Keinyama au Kupekecha Msasani. Redi Aizi kitu gani bwana?ntaibuka we ncheki maeneo maeneo hapo ila tusikerane.
0713374649

Friday, February 1, 2008

Fabio Capello ambania Beckam


KOCHA wa England, Fabio Capello amempiga chini
David Beckam kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya
Switzerland jumatano ijayo. Mashabiki wengi wa nchi hiyo wamekuwa wakimtaka Capello anayepuuza mambo na kushikilia misimamo yake, kumpa nafasi Beckam ili atimize mechi yake ya 100.
"Nimemshauri kwamba yeye ni sehemu ya mikakati yangu na atakapocheza vizuri zaidi Marekani nitamuita,"alisisitiza Capello mwenye miaka 61.