Thursday, October 18, 2007

Msikieni Banana Zorro anavyosema

Msikieni Banana Zorro anavyosema
......... Hii ni laivu amelonga na Mzee mzima hapa.

"Kinachotokea ni kwamba wasanii wengi hapa kwetu hawajaelewa umuhimu wa kutuma kazi zao kwenye kituo kama Channel O, kuna vitu vingi vinachangia lakini mi nafikiri ni uelewa binafsi.

"Halafu kwenye suala la ubora bado, wasanii wanaiga mno kila kitu kutoka nje hususani Marekani, sasa mwisho wa siku wanashindwa kuzipeleka nje kwa vile hazina jipya wala hazitofautiani na hizo zinazotoka Ulaya,"


"Unakuta msanii ana wimbo mzuri lakini ikifika kwenye suala la video anaiga kila kitu, hakuna jipya yaani, halafu na makampuni yenyewe ya kutengeneza ndio yale yale, sasa zinavyopigwa zinakuwa zinafanana kwa kila kitu na ile halisi ambayo pengine unakuta ni ya msanii mkubwa ambaye amejijenga sana.

"Silaumu watengenezaji, wasanii ni tatizo kwa vile mtu unapaswa kujua kwamba unataka nini na ufanye nini, unakuta msanii anaiga mawazo na mfumo wa video ya Kimarekani ambayo imeandaliwa shilingi labda milioni sita lakini yeye anataka kuitengeneza kibongo bongo shilingi laki tano au sita.

"Unategemea nini hapo? huwezi kupata kitu makini na huu Umarekani ndio unatumaliza kabisa tunashindwa kushindana nje na wenzetu kwa vile hakuna jipya, ndio hiyo inatokea Channel O unakuta yupo mmoja wakati bongo hapa hawana idadi.
"Matokeo yake ndio unakuta wenzetu wanazidi kupeta tu sisi tunabaki na Bongo yetu,"anasema msanii ambaye haya dingi yake ni Mwanamziki kama ulimskiaga kwenye ile Mass Media Bendi ile iliyochanaga na kupotea ghafla kila mtu akala chake.

No comments: