Saturday, October 27, 2007

Banza ni mkwara au kweli?


MWANAMUZIKI Banza Stone ambaye ni kiongozi wa bendi ya Bambino Sound Original, aliyoifufua hivikaribuni amesema kuwa anasuka bendi imara na itakayokuwa mfano wa kuigwa Tanzania.

Banza aliifufua bendi hiyo wikichache zilizopita baada ya kujitoa Twanga Chipolopolo na tayari ameshaanza maonyesho ya utangulizi ingawa anatazamia kufanya uzinduzi Novemba 3 jijini Dar es Salaam.

Msanii huyo alisema kuwa anakiamini kikosi alichonacho hadi sasa na ameridhishwa na kiwango cha kila msanii lakini anajipanga zaidi kuhakikisha anakuwa na msingi imara.

No comments: