Friday, October 12, 2007

Nendeni mkaone ya Sangoma

NAHISI vitu vingi.. vingi.. vingi… vingi, vinginee sivisemi hadharani!Utasema nini wikiendi kama hii ambayo kila kitu segemnege?. Kila mtuanajifanya yuko bize hata katika mambo mengine ambayo hata hayamhusu. Utawaambia nini siku kama hii ambayo kila mtu ni Rais wa Yanga auMwenyekiti wa Simba?. Ni mapambano ya ubabe juu na chini ili mradikieleweke.Jamaa wa mazindiko na wazee wa Kamati za ufundi ndio wakati wa kuneemekakatika harakati za kuhakikisha ushindi unapatikana kwa njia ya Sangoma. Ninoma!.Huko uswazi ardhi za makaburi zinapata taabu kutokana na mishughuliko yahao Makomandoo na wazee wa fitna ambao wamemua kuhama kabisa uraiani etikuweka mambo sawa!.Unashangaa? Siyo makaburini tu hata Kunguru na mayai yake yamekuwa dilimtaani. Wamegeuka zana muhimu kwa wazee wa shughuli baada ya Kuku nafamilia yake kugeuka bidhaa adimu.Hata mateja yaliyokuwa yakinyaka jiti jiti na kupayuka huko kwa MamaZakaria wamesarenda na kuanza msako baada ya kushtukia dili la Kunguru kwaSangoma.Lakini Mzee wa Kutibua alipocheki na Wanyetishaji fulani kutaka kujua kwanini hao Kunguru wamekuwa ishu? Wakajibu eti uzoefu unaonyesha kwambahawana mapozi na wanapenda kujihusisha na majukumu yasiyowahusu . Duhlahaula!.Wabongo? Hakiyanani ni soo. Hakuna tena ufundi wa mpira uwanjani bilamkono wa Sangoma au kuwatoa mhanga hao Kunguru wanaotusafishia hiyoKinondoni huko kwenye jiji la Kandoro. Hao makocha wapo wapo tu kama ushahidi kila kitu kitambooo kamati zawazee wa shughuli zimeshafanya. Utaona mwenyewe.Unabisha? Shauri yako. Wenye mpira wao wanahesabu masaa iwadie hiyo keshomtu mzima aumie kwenye uwanja wa Jamhuri huko wanakoita Morogoro ambakowanataka eti kuwe na Bahari.Watu wazima sema Simba na Yanga ukitaka, wamepenya kwenye hiyo iliyokuwaikiitwa Sita Bora na sasa wamedondokea fainali kumtafuta mbabe wa soka laBongo kwa 2007.Hao jamaa kila mmoja tayari kashapata nafasi ya kushiriki hiyo michuanoya Kimataifa huko mwaka unaokuja lakini ishu ya kesho ndiyo itakayoamuanani aende kwenye hiyo Ligi ya watu wazima. Aah! Sore. Ligi ya Mabingwa namwingine kombe la Shirikisho.Lakini kazeni buti washkaji kesho tunataka kuona soka ya ukweli ukweli, yautu uzima siyo ubabe au misifa ya kijinga. Mzee wa Kutibua na washirikazake wanaibuka kuja kuona soka siyo ngumi.Chezeni mpira hatutaki aibu, onyesheni dira ya kweli kwamba nyinyi ndioSimba na Yanga kweli ambao ni wakongwe wa soka ya Tanzania ambao ni zaidiya hao maswahiba wenu ndio maana mkatinga fainali.Futeni hizi ishu zinazosemwa huku uswahilini kwamba mmebebwa na hao jamaawanaopuliza hizo firimbi. Wanaitwaa… dah! Nitakuambieni badae nimesahau.Wala hatutaki kuona mavurugu yasiyo na maana kama ilivyotokea kwenye hizomechi zilizopita na jamaa fulani fulani kujikuta wakijisaidia ndoo.Ukiacha ishu ya ubingwa, si suala la kuuliza umuhimu wa mechi ya hao jamaakila wanapokutana. Ni mshikemshike ambao huibua mambo mengi.Kila mdau wa soka anataka kuona viongozi wakiwajibika na kutumiaustaarabu wa hali ya juu kuhakikisha mechi inachezwa salama na kila kitukinaenda salama bila rapsha.Viongozi wanapaswa kufanya kazi kama viongozi, si kugeuka makomandoohatutarajii kuona viongozi wenye heshima zao wakisukumana na mashabiki aukupigana au kuendekeza imani za kishirikina kama rekodi zinavyoonyesha.Au hamjiamini? Sasa kiongozi akigeuka mchochezi wa vurugu mnategemea ninikitakachofuata kwa hao wanaojiita Simba damu au Yanga damu.Tubadilike wakubwa. Twendeni kisasa mambo ya kubeba tunguri na zananyingine za Sangoma ni kujiaibisha, waachieni maticha na hao vijana wapigekazi.Kila timu iko fiti na ni nzuri kwa maana ya wachezaji na ushindi unawezakupatikana kwa akili na maarifa ya kiufundi ndani ya dakika 90 za kawaida.Ni jukumu la walio shikilia makali kuhakikisha hata mashabikihawasababishi vurugu zisizo na maana kama ilivyokuwa ikitokea katika mechiza Simba kwenye Ligi Ndogo.Na Polisi nao waache ushabiki. Hayo siyo mambo washkaji ndio hatukataikwamba suala la ushabiki ni haki na uhuru binafsi wa kila raia lakinikatika hili kuweni makini.Acheni hizo ishu wakubwa. Nyendeni uwanjani kuangalia mambo ya usalamamambo ya unazi ni baadaye, jukumu lenu ni usalama si ushabiki.Mzee wa Kutibua hawaonei lakini rekodi zinaonyesha washikaji kwamba majihuwa yanazidi unga. Si tumewashuhudia huko kwenye uwanja wa Taifa hatahapo Morogoro mara kibao tu. Kwanini msiige wanavyofanya wenzenu waRwanda?.

No comments: