Friday, October 12, 2007

Maximo amewatenganisha na ukuta

BALAA hili sasa lashakuwaa..., kubwa kabisa tena zitoo au njama zenutulikimbie jijii.. mwajua ni noma lakini bado mwakandamiza.
Kabisa kabisa tena hata aibu hamuoni mwathubutu kusema bila haya tenamwachekaa.. "karibu tena anko" kwa lipi hilo?.
Mwataka ndondi.. au?.Twazijua sisi mpaka za kijapani nini za kichina china bwana !.Au ndo labda mwataka tuumbuke tusiende haja siee.. tubaki kupiga miyayotuu... kutwaa? Wengine deshi ndio zetu lakini tukizifuma ndio hivyotwaanzia kwenu sababu Pilipili na ndimu Kempiski siku hizi hakuna bwana.

Hakuna! Waziweke za nini wakati wenyewe wanywa vya kwenye makopoyaliyoning'inizwa kwenye hayo majokofu? kule kwetu Ipagala tunaitagaFuriji.Nyie Dizeli na Petroli zakuhusuni nini? au ndio kweli tuaminimwakorofishia viepe? mnatuambia bajeti imekwea, hiyo kitu inahusianaje naPilipili za shingi shirini!Finyango tatu. ..tatu kabisaa... wani...twu...sriii... na maji yakuchemsha (eti mwaita supu?) . Ya kuchemsha kabisamaji tena ya kisima ndio maana matumbo hayatuishi Bongo. mwatuuzia bukuu..!.Huyo wanayemuita Mama Megji mkoba wake umezua balaa huku bongo kila konawimbo ni ugumu wa maisha.Hali imekuwa tete, jua limekuwa kali kupita kiasi mifukoni hata kwa Mamantilie ambako masela walikokuwa wakiponea kwa ugali wa 300 mambo yamekuwasi mambo.Hata vyumba vya buku mbili shin tanu uswahili hakuna tena, zile tabasamukwa washirika wa Mzee wa Kutibua zimepotea na kauli mbiu imekuwa mpakakieleweke.Lakini baadhi yao kama kina Munyuku huko Kijiweni wameanza kuvuta hisia zamaisha ya Vibatari umakondeni sababu muda chi nlefu chafali itawadia.Ndio hivyo! mambo yamebana kasi mpya imegeukia kuunguza waleti sasa naniasubiri kuumbuka auche chuluali.Atabaki nani kwenye hili jiji ambalo siku hizi watuletea mpaka mabinti wakutukogesha kwenye hizo Saluni !Jamaa zinaingia kunyoa sharubu lakini wanagairi wanaanza kukaruza paraili wapate sevisi za hao mabinti mpaka wasinziaaa... kwenyekinanihiii.....kiti. Amah!Kabla sijasahau! kuna jamaa wanakwea pipa leo na kesho twaskiaa...wanakwenda kupiga matizi kwa Wazungu. Dennark na Uswisi.Nyeti alizopata Mzee wa Kutibua laivu toka huyo bosi wao, Mbrazil, MarcioMaximo ni kwamba hao mabwana wanakwenda kusaka makali ya kuwachapa haoWamakonde waite Msumbiji ukijiskia. Huko kwenye dimba la Taifa Septemba9.Oya washkaji hilo shavu hilo. Tumetumia mamilioni ya shilingi ilikuwatengenezea mazingira ya kila aina kuhakikisha mnatupa raha wakubwa,tunataka ushindi tu na tuende Ghana mwakani.Siyo mara ya kwanza hii, miezi fulani fulani hivi siikumbuki tuliwapelekahuko wanakoita Brazil kuwasuka sitaki kufunua mlichofanya baada ya hapo,lakini lazima mtambue tunawapeleka Uzunguni safari hii mkajifue.Hatujawapeleka pikiniki au kushangaa wazungu au magari yenye gorofatunataka mkajifunze na ni nafasi pekee ambazo hazijirudii. Maximoamewatenganisha kwa ukuta mwepesi sana na hao wenzenu huko nje yakikosi. Angalieni wanavyotoka jasho wakiwania hizo nafasi fanyeniupuuzi mjione mastaa abomoe huo ukuta mje mle msoto.Uliyepata nafasi ya kuwa kwenye msafara wa mafunzo jiulize na ufanye kilakinachowezekana kuonyesha umahiri wako Ulaya ni sokoni. tumieni hizomechi za kirafiki kuwahamasisha mawakala wa kimataifa .Kwa jinsi kikosi hicho kilivyo kila mtanzania kama alivyo Mzee wa Kutibuaana imani kwamba Stars itafanya vizuri na kuandika ukurasa mpya katikasoka la Tanzania kwa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa kuichapaMsumbiji na kufikisha pointi 11. Tujitutumue tuwapige kwanza mengiyatajulikana juu kwa juu.Tumechoka kuwaangalia kina Drogba, Lampard au Essien kwenye kideo,tunataka tumshangilie Haruna Moshi au Saidi Maulid akiwa jijini Accra naFerguson wa Manchesta au Mourhino wa Chelsii akae kwenye sofa na wainiyake awashangae wabongo wanavyokipiga na Cameruni. Alaa?Kila mtu afungue akili yake azingatie maelekezo, hayo mastarehe yapo tumtayakuta, kama ni hela zipo tu hata kabla hamjazaliwa na haziishi milelena mileleni. pigeni kazi washikaji.

No comments: