Friday, October 12, 2007

Tiefuefu inavyoshikwa masikio

“MKOROFI nanii.. nani alaumiwee hee heemwaka wa shetaniiii…,nanii alaumiwee eee ee..Akilini mwangu mii nawaza, nakumbuka wapi tulipotokampaka leo tunavunjikaa…”Mzee wa Kutibua vipi leo? Au mkwara? "sijuii", pengine biti zimemdatishakwa Dunga, “Sijui”, au mambo ya mwisho wa mwezi? “Sijui”, labda kadata,“Sijui”.Ni maswali yanayowakaa kooni washirika wa Mzee wa Kutibua mida kama hiiwanapoperuzi ukurasa huu kutokana na vesi matata aliyoanza nayo ambayo sikawaida alivyozowea kusomeka.Lakini si uungwana kwa Mzee wa Kutibua kuanza kumwaga sera kwa washirikawikiendi hii bila kuwapa hai kimtindo kuweka mambo sawa ingawa bichwa lakehalijakaa freshi.Limejaa nyeti za kumwaga, ndio maana minywele haikai inabaki kushindilianahuko kunako kidevu jirani na domo ambalo siku hizi limekuwa likimwagabusara za kumwaga kwa mabwana wadogo huko Dasilamu mjini.Ndio mambo yenyewe ya tawni wenyewe wanasema Kibongo Bongo, kila jambolazima liwe na mikogo yake. Ndio maana hata kina Sera wameamua kung’oamabati yote kwenye hayo mabaluni na kutembelea Chesesi.Wameamua na wenyewe wabuni yao, kwani hujaona mpaka wengine siku hizi hukoShamba wanakoita Tegeta wanatinga Naiti klabu na Fusso? Wenyewe siku hiziwanaita “Flying Beds”. Aliyekuambia wanataka vigari vyenu vya kubanananani?Zao makulaji, mitungi kwa sana, kujirusha na hizo Banjuka za kina DNA hataMugongo Mugongo ngoma ikizima wanatoka nje wanaegesha kwenye Fussopanakucha.Wanyetishaji wamembonyeza na Mzee Kutibua na kumpa mchapo mpya kwamba sasaukitaka kujizolea maujiko bwana kuliko hata bwana mkubwa JK huko StetiHausi uitwe Mdebwedo.Unaweza kujikuta ukikusanya mtaa mzima ndani ya sekunde moja na utaonahata magego ya wanywa gongo ambayo siku hizi yamekuwa kivutio chawazururaji. sore Watalii. Kwani we hujaskia wengine wameanza kuhifadhiwahuko Bwagamoyo.Hao jamaa acha bwana wamejigundua kwamba ni dili ndio maana siku hizi hatawakicheka wanaziba midomo na mashati. Siku hizi Mzee wa Kutibua kaambiwahuko Tazara kwa kina Masanja wamekacha kupanda hata daladala wanazuga etini mgomo baridi kupinga hizo nauli mpya.Lakini washikaji ishu zingine lazima ifike sehemu tukubali kuwa na watuambao wana misimamo kwenye maamuzi na kuachana na ushabiki wa kizamani nakuangalia majina. Ebu niambieni, kwani hao wanaoitwa Simba na Yanga ndio kina nani kwenyenchi hii ya wadanganyika ambao hiyo Gavamenti inatuambia wanafika ‘emu34’, ukiondoa vidume wawili wa Mzee wa Kutibua walioibukia kwenye uso wadunia miezi kadhaa iliyopita ambao eti ndoto zao ni kuwa na sharubu kama Dingi yao.Kwani lazima mashindano yoyote ya nchi hii zishiriki hizo timu za hukoMsimbazi na Jangwani? Ni maswali anayojiuliza wa Kutibua ambaye kamawalivyo wadau wengine alikuwa akisikiliza mikwara ya hiyo Tiefuefu naSimba huko kwenye hivyo mnavyoita vyombo vya habari kuhusu Kombe laTusker.Simba ilikuwa miongoni mwa klabu sita zilizokuwa zishiriki michuano hiyoinayoanza leo, sijui pengine ni kwanini. lakini baada ya michuano hiyoambayo awali ilikuwa ifanyike kwenye uwanja wa Taifa kushindikanaviliibuka vitimbi kibao baina ya hiyo Tiefuefu na timu Simba na Yanga.Kitimbi cha kwanza kilichoibuka ingawa kilionekana kukomaliwa zaidi naYanga huku Simba wakiwa wanajifanya wameuchuna ni kutaka zipewe nafasitatu za kusajili wachezaji wapya.Yanga ndio ilikuwa mstari wa mbele kutishia kujitoa kwenye michuano hiyoendapo isiporuhusiwa kuongeza lakini ghafla bila kujali kwamba awaliwalikuwa wameshakubaliana kwamba kila timu itatumia wachezaji 20wanaocheza Ligi ya ndani, Tiefuefu ikafyata ikakubali wachezaji waongezwengoma ikatulia.“Ninachosema ni hivi mashindano yanachezwa kwenye uwanja wa Taifa,” nikauli ya jamaa mmoja wa Tiefufu ambaye yeye akiwekewa kinasa sautianachojua ni kupayuka tu. Badae nyasi bandia zikashindikana kutolewabandarini kwa muda muafaka akaumbuka. Tumwache.Vitimbi vikaendelea akaibuka Simba, anachosema haendi kwenye uwanja waJamhuri huko Morogoro ngoma ilikohamishiwa mpaka apewe milioni kumi keshikwa mechi zake mbili za kwanza, anachodai Morogoro hakuna mapato.Tiefuefu ikaangaika kukaa na Simbaa… lakini mwisho wa siku waandaajiwakaamua kumaliza ubishi. Klabu zikakutana na wadhamini kwenye kikaoambacho Simba waliwakilishwa na mabosi wawili wakafikia muafaka mashindanoyahamie tena Mwanza.Mashindano yakahamia Mwanza Simba wakageuka maamuzi yao, wakagomahawaendi Kirumba wanataka kubaki Morogoro. Tiefuefu ikaanza kuchachawatena inakaa na Simba kuibembeleza ishiriki.Ndio! sibishi kwamba Tiefuefu inapaswa kukaa na mwanachama wake kuwekasawa baadhi ya ishu za msingi lakini inayumbishwa mno. Aibu gani hii yaunazi wa Simba na Yanga?.Huku ni kuyumbishwa na kushikwa masikio kwa Tiefuefu, haiwezekaniviongozi wenye akili tena sio akili tu timamu, wakubaliane jambo halafubaada ya muda wabadilike kila atake mambo yaende anavyotaka. Basikusingekuwa na haja ya kuwa na chama.Simba hataki kushiriki kwanini mumbeleze? Mmekubaliana kwa kanuni kwa niniTiefuefu msiwe na msimamo mmoja mnabaki kufuata nyayo za rangi tu? Wenyewewanajua wamejitoa kwa nini waacheni.Kwa nini myumbishwe na kikundi cha watu wachache wenye malengo yao? Ndiohay ohayo inafika mwisho wa siku kunafanya Tiefuefu au baadhi ya viongoziwake kudhalilika na hata kutawaliwa na watu wachache.Tiefuefu ifanye kazi kwa kutumia makucha yake, sheria hazikutungwa kuwekwakwenye maktaba au madroo ya hizo. Kila timu kinapaswa kwenda kwa haki ilikuepuka kukandamiza klabu nyingine ambazo siogopi kusema kwamba hazinakauli.………….

No comments: