Friday, October 26, 2007

Nyie endeleeni kama hamjala za uso

KULENi tano! Wanangu wote mnaonicheki maeneo haya ya kujidai mida hii, mimi niko pisi sana masela na maishu yanaenda kimtindo mtindo.

Si unajua tena laifu la kiutu uzima linavyokuwa mvi zikishatanda kwenye injini ya juu? Ni kukomaa na vijana wa siku hizi ilimradi ukitinga jioni makidi wapokee kitu kumkono waringe kwamba na mshua wao kumbe zimo, si unajua za kivile?

Mwanangu mtu mzima ukiibuka na maulaji ulaji, basi striti yoteee... ngoma iko hewani vibaya sana, mpaka mtaa wa saba kwa kina nanihii wanajua jamaa mambo safi. Si madogo washafikisha, ndio usupastaa wa mtaani kwetu huo wana.

Kidogo kidogo tayari ushaingia kwenye sistimu na mambo fulani yanakaa poa Bongo, mkwanja unaanza kumwagika, madili kwa sana tu! sio ishu kupiga mayenu mpaka shingoni ukatize site senta na mabaunsa kibaa...oo!

Mkwanja kibao unahangaiika…! Si uite masela uwapige mtungi wa maana wakupage ramani kibingwa tu..!

Simpo kichizi, wala si lazima ukauze sura Bilzi kwenye dansing floo uibue vagi ukawafaidishe machizi wanaochukua dondoo za manyuzi ya udaku, halafu moningi ukaanza kuona soo kuibuka kwa wakwe.

Sam taimsi ishu tafu bongo lakini ndio ivyo wani deyi yesi, ingawa wanangu fulani wa yelloo Jangwani wanadai Sa Godi anawatupa kichizi, anakuwa kapiga zake pono lile la fofofo kila wanapokutana na hao swahiba zao hapo Msimbazi.

Mei bi wanamaanisha mambo yameendelea kuwa mazito, lakini siyo kiivyo, mbona mkwanja kibao tu unamwagika evuridei mpaka vijana wamechafuka dolerii...?

Au kuna samusingi kilitokea mitaa ya Jamuhuri Stadiumu ? Mzee mzima ayi donti no enesingi bwana! Huwaiii… Kwanini, lakini!

Lakini machizi kama vipi iti izi beta samtaimzi kusteyi kivyako vyako kama Mzee wa Kutibua na Tukuyu Stars ya kijijini kwao, hayo matimu ya kina nanihii presha tupu. Boli lenyewe la kibongo miyeyusho tu hili, mkwanja kibao bado mtu mzima unateseka tu. Huwaiiii…!

Lakini ebu kula ganzi kwanza kidogo nikuambie kitu, nyeti za vijiweni ntakupa baadae kidogo. Kwanza tuwape shavu Yanga kwa kunasa makocha watasha ambao tayari Mzee wa Kutibua na wenzake waliokuwa wakiangalia runinga wamewashuhudia wakishuka hapo kwenye hicho kiwanja maeneo ya Vingunguti.

Halafu isitoshe tukawaonyesha laivu ndani ya Jamhuri Stadiumu juzi. Masivii yanaonyesha ni bonge ya matekinishiani wala Mzee wa Kutibua na wadau wengine wa soka ambao kwa nyadhifa zao wamepata nafasi ya kuperuzi hawana noma ndio maana hatujawasoma wakibonda.

Ingawa bado hatujaambiwa kama Waserbia hao, Kondic Dusan (Mkuu) na Spanso Solokovski hatujanyetishiwa kama wameshamwaga wino kwenye kontracti lakini viongozi wa klabu hiyo pamoja na wanachama wana kazi kubwa ya kufanya.

Ujio wa hao madingi (wako kwenye siksite samsingi kwani hujui!) ni mwanzo mpya na mzuri wa mafanikio kwa vile wana uzoefu na nchini za kiafrika, lakini haimaanishi kwamba ndio kila kitu tayari.

Miezi si mingi jamaa mmoja mzungu walikuwa wanamuita Micho naye alikuwa mitaa hiyo ya Jangwani lakini pamoja na uswahili wake, akaingia mitini kiaina na kumuacha kila mmoja akisema lwake.

Lakini huyo mzungu ambaye mashabiki wengi hawakudhania kwamba angeweza kuchomoka veere suuni…, baada ya muda aliibuka kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti hili akidai kwamba anataka kufanya kazi kwenye klabu ambayo yeye “atatekeleza majukumu yake ya kiufundi tu kama kocha kuliko kuhangaika na mambo mengine”.

Kauli hiyo pekee imebeba maana nyeti ambayo viongozi wa Yanga wanapaswa kuifanyia kazi na kujipanga upya kwa kutengeneza mazingira mazuri ya kazi ambayo yatasaidia wataalam hao wanaolipwa ghali zaidi nchini kuweza kutimiza malengo yao.

Vinginevyo mamilioni wanayolipwa yatayeyuka na yatakuwa hayana maana kwani zoezi la kuingia mitini lililowahi kufanywa pia na makocha Wabrazili wawili wa Simba hata na Msauzi Trott Moloto yataendelea.

Si wakati wa viongozi kuendeleza migogoro ya ndani kwa ndani ambayo inaweza kuvuruga wachezaji na kuanza kuhujumiana. Ni wakati wa kujenga mustakabali mpya haswa kwa kuangalia Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa mwakani, tumechoshwa na hadithi za 'haikuwa bahati yetu'.

Wachezaji nao watunze vizuri na kusiwepo na matabaka ambayo yanaweza kujenga hisia wala mianya ya mkato wa tamaa.

Wanachama na wenyewe pia wanapaswa kuacha chokochoko zisizo na msingi na kuzingatia zaidi maslahi ya wengi, kuanzisha vurugu kwa lengo la kuitwa na kibosile fulani upewe kitu kidogo haijengi na hii si karne ya kuishi kwa kutegemea klabu, badilikeni.

Hata mashabiki na wenyewe wasitegemee mambo ya mteremko na waache jazba, wabadilike wawape nafasi wataalam wafanye mambo yao, wao wabaki kushangilia jukwaani tu.

Haya bwana! tuishie zetu kwenye minuso ya wikiendi, wenye uroho wa kitimoto kama Munyuku (sijasema!) wapige kwa tani yao kama Mgiriki huko Meeda ambao kwa mujibu wa kalenda ya Mzee wa Kutibua siku kama hizi bado ni muafaka za kutumbua kilaji mpaka majogoo.
Lakini msifogeti pia Zee la Kutibua lipo kwenye blogu; zeewakutibua.blogspot.com) ingawa wanazuoni waliojitolea kufanikisha zoezi hilo wanamuambia bado mchakato unaendelea muda si mrefu everisingi will bi oluraiti bila chenga.

No comments: