Tuesday, January 29, 2008

Twiga Stars wana uelewa mdogo-TFF


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema uelewa mdogo wa wachezaji ndio uliosababisha kutishia kugomea kambi ya timu hiyo iliyopo kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela alisema wachezaji hao kwa upeo wao walidhani shilingi milioni 2 zilizotolewa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete ni motisha yao kwa kuwafunga Eritrea.
"Uelewa wao mdogo ndio walitaka kugoma, walidhani zile hela zilizotolewa na Mama Kikwete ni zawadi yao walipoifunga Eritrea."alisema Mwakalebela ambaye ana kitambi.
"Zile fedha zilipoletwa nilimwambia meneja wao awalipe posho yao yote pamoja na walimu zilibaki laki moja nikamwambia ajaze yote mafuta basi la wachezaji linalowapeleka na kuwarudisha mazoezini.
"Mama Salma Kikwete alipotoa zile hela alisema ni za kuisaidia timu katika maandalizi yake dhidi ya Eritrea sasa wao kwa upeo wao sijui walivyoelewa wakahamasishana wakataka wapewe zile hela zote wagawane kama motisha wao wa Eritrea."

No comments: