Tuesday, January 29, 2008

Oya mshikaji Ulabu gani huo...?

ANGALAU! Lakini dah! Sijui itakuwaje masela, kuna ishu ishu fulani ambazondivyo sivyo kimtindo kwa mwanenu, inabidi tuteme mate chini tu.
Kakikohozi kwa sana na wese linashuka kichizi puani tangu juzi kati hapo,sijui ndio inakuwaje tena mambo kama hayo kwa mtu mzima kama hivi.Au huyu msela hapa kulia anafanya mambo fulani nini nimwachie liuwanja lakujinafasi?
Mambo yamekuwa mazito ikabidi watu wazima wamrudishe bwanamdogo bushi kidogo akaweke mambo sawa. Lakini sio ishu tujifanye hatujui.Basi juzi kati fulani bwana, mida ya jioni nikaibuka zangu mitaa yaUbalozi (jirani na hiyo klabu wanaita Lidaz) kule Kinondoni kwa nyumanyuma hivi sehemu fulani wanaita Octa Contena wanakoutwika wajanja.

Nilikuwa na mtu kama tatu zenye nyadhifa zao kwenye ofisi nzito nzito hukotawni ambao hata kuvusha wiki wakiutwika ‘twenti fo Awaz’ na kuegesha juuya meza kwao siyo ajabu.
Wakati watu wazima tunazidi kujinafasi na mamonde yaliyotanda zake mezani,kumbe bwana meza ya pili kuna masela fulani hivi kama wawili (nimetonywani Mapaparazi wenye maujiko ya kufa mtu Bongo hapa) mmoja kautwika zakemadude fulani hivi yanakaa kwenye maboksi(wanaita Penasoli sijui…kitu kamahicho) nafikiri kuanzia moningi jamaa anayagonga tu kwa mujibu wa wadau.
Kuna vagi kimtindo jamaa anakuja juu, hata macho hayataki tena kuona, basimwana mida hiyo masela huku pembeni burudaani… jamaa kazidiwa kanyanyukakwa msaada anaoujua mwenyewe kaibuka zake toileti.
Ni mida fulani ya saa mbili na ushee, masela zake wakangoja wee bila bilawakadhani labda jamaa kamwagiwa tindikali na Mafisadi au Jamaa fulaniwaliolamba mabilioni ya Biotii wamemzamisha toileti ili azibe mdomo,ikabidi wamuibukie.
Kumbe bwana msela maji yamezidi unga alipotoka zake kupunguza Toi,kasahau alipokuwa ameegesha kapapasa papasa geti la uani katokea Baa yajirani nako bado chaneli ikawa haikamati akaamua kutoka nje akaegeshakwenye lami ya Alhassan Mwinyi.
Duh! Blaza vipi tena?Mungu saidia Dada nanihii katafuta kichizi kila mahali kakosa,alipobahatisha Baa ya pili akaambiwa kuna msela alipita na ukuta hapamcheki labda rodini. Duh jamaa akanaswa bwana kaegesha rodinialiporejeshwa kwa masela wake anacheka mbavu hana…, nini kisa eti alijuayuko kwenye taxi anaenda Mwenge.
Duh! Blaza inakuaje ukinywa za uswahili?Uchune kidogo nikuambia ishu nyingine. Kiligi chetu cha Bongo ujuekinaanza leo kimtindo, wenye kupenda lahaa… tunaibuka zetu badayegraundini tukaangalie boli la wanetu siunajua tena tulikuwa tumelimisimida?
Lakini wana mmepiga matizi mwezi na ushee hatutaki kuona madudu na ushenziushenzi usiona na maana kama ilivyokuwa kwenye mzunguko ulijikata mwakajana ambao watu wazima Lunyasi na Jangwani walikiona cha moto kwa haowaliokuwa wakidhani ni mabwana wadogo.
Ubabe siyo ishu badilikeni wanangu, pigeni boli la akili kama tunalochekikwenye kideo huku Ghana, mangumi na kukanyagana kanyagana sio dili. Ndiomaana mnazidi kubanana Bongo tu na utajiri wa kutembelea Baluni na vyumbaviwili uswahilini.
Badilikeni mchezee mpira si miili ya watu, tumieni akili na vipaji vyakuzaliwa wazee sisi tunatoa mkwanja wetu hatuji kuuza sura tunakata kuonagemu tufurahi na magoli yafungwe si papara za ajabu zisizo na akili.Tulizeni akili msikilize mnachoambia na Maticha mtufanyie mambo, sisimkiendekeza ishu za ovyoovyo kama lasti raundi sisi tutakupigeni chini tukama vipi.
Tunakaa Baa tunapiga zetu ulabu na kuangalia kina Drogba, Eto’o na Kanuti. Haturembi simnajua zetu!Msiwe mizigo washikaji fungueni akili kuna ulaji kinoma Taifa Stars,muonyesheni mambo Maximo mle shavu na soka yetu ikue.
Ndio tunachotaka,ishu za ujiko ni baadae.
Ndio wakati wa kutuliza akili, kucheza na kuachana na mambo ya ajabu.Halafu kitu kipo laivu kwenye kideo cha Gitivii mjue! Ndio nafasi zenyeweza kujiuza nje hizo, onyesheni kujiamini mbona Kenya na Uganda wanaibukanje kibao na kufanya mambo kwani wenyewe wana miguu ya plastiki.
Acheni papara na anasa zisizo na msingi hiyo ni kazi wakubwa, tumieniutashi kuweni na ari ya mabadiliko tunakokwenda ni kugumu kichizi na umriunazidi kuyeyuka.Imefika enzi za wachezaji kubadilika na kuishi kama binadamu wa karnempya, msiridhike na maujiko ya uwanja wa Taifa mabega yakazidi vichwamkasahau kwamba kuna leo na kesho na maisha yako kama mchezaji yako miguu.
Kwamba mchezaji unaweza kuwa na mafanikio wakati ukiwa kwenye fomu keshona keshokutwa mambo yanaweza kubadilika. Na hivi wakazidi kuingia makochaWazungu patakuwa hapatoshi mkiendekeza uvivu na usupastaa wa kununuliwaKilimanjaro Uswahili mtaona Bongo chungu.Mtajichuja.
Na kwanini ifikie hatua hiyo? Wakati mna kila kitukinachostahili kwa nyie kibadilika na kufikia kwenye hatua inayokubalika.Oya washikaji pigeni kazi, embu jiskieni haya kidogo basi tupige na sisihatua kimataifa, kwanini mashabiki wenu wawe wawe wapweke kila sikukomaeni mtuinue Wabongo wenzenu wana.
Nasi tucheki wani dei. Mwanangu Songoro mitaa ya Chaga Baiti, Wili kwa Mapecos hapo na Wazee waNewvision, Sayansi kwenye kitimoto sana… tu! Leo Mtaumia, Mcameruni wenuatachomoka kwa Zambia iliyompiga Sudan tatu kwa mtungi?

No comments: