Tuesday, January 29, 2008

Aisha Madinda:Wameniambia niokoke nipone


“Nimepokea simu kwa mamia na meseji nyingi sana, ila kuna wasamaria wamekuwa wakinishauri mara kwa mara kwamba niokoke na kumrejea Mungu kutokana na hali niliyonayo.
“Wanasema kwamba endapo nikifanya kitu kama hicho naweza kupona haraka na kurejea kwenye hali yangu ya kawaida mapema kila mtu amekuwa akitoa maoni yake na nimekuwa nikiwaskiliza.
“Lakini bado sijaamua nini cha kufanya bado nataka kuzingatia matibabu ambayo nitakuwa napewa na madaktari wa Muhimbili kwanza halafu nione nini kitakachofuata lakini nina imani kwamba ipo siku hali yangu itakuwa vizuri,"Aisha alimwambia Mzee wa Kutibua jana jijini Dar es Salaam.

Mwanamama huyo mwenye watoto wawili wanaosoma sekondari amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya moyo kujaa maji na miguu yake sasa imevimba kiasi kwamba anashinda hata kuvaa viatu wala hajaenda kwenye maonyesho kama miezi mitatu sasa imepita. Baaadhi ya wanyetishaji wasio na dogo wamekuwa wakiihusisha hali yake na imani za kishirikina.

No comments: