Friday, November 23, 2007

"Leaders of conflict and gate collection"

WASHIKAJI mambo vipi hapo! Mwanenu nipo freshi kimtindo ingawa bongo kimechafuka kinoma wanangu. Joto kichizi wenye ngozi za vyura tu ndio wanaopeta.

Sijui ndio kiama chenyewe kinaanza kubipu bipu kiaina maana wenye jiji letu hatuelewi elewi jinsi ngoma inavyovuma kila panapoguswa hali si shwari.

Ingawa mambo fulani ni shwari wanangu wa Lugalo soo soo.. kabisa! Sijui ni ushamba au labda kwa vile ni mara kwanza kuwaibukia ebu tuwachukulie ndio fasheni.

Ngoja sasa nikupe ishu yenyewe! Mzee mzima kama kawa mambo ya kujirusha mitaa ya Bongo wikiendi siunajua ndio zake? Sasa wikiendi hiyo iliyopita masela kama saba hivi wenye nyadhifa zao wamejimwaga naiti klabu moja hapa mitaa ya Lugalo kama unaenda Tegeta. Wenyewe siku hizi wanaita Bondeni.

Wadau wakamuendea hewani Mzee mzima nikaibuka eneo la tukio tayari kushusha kitu sehemu fulani huku ukihudumiwa kama ‘Presidaa’ kutokana na unyeti wako kwenye eneo la tukio ambalo wamo jamaa wenye minoti yao ya kusumbua tawni fulu taimu.

Kuna makelele mengi humu ndani lakini baadae jinsi muda unavyokwenda unakuja kugundua kwamba kuna kikundi kingine cha jamaa kama sita kwa nyuma yenu ambao karibu wote ni kutoka kwenye hii jamii ya jamaa fulani(ya kanda ya ziwa wananihii…) ambao wanajifanya Inglishi ni sehemu ya laifu yao toka Kileji.

“Ofukozi Rwego (Rwegoshora) mpe coldi wani, halafu athazi ai don rimemba” ni kauli ya mmoja wa hao jamaa kwenye hiyo meza iliyojaa kina Rwechungura, Kaijage na wengine wengine (nimewasahau).

Baadaye kidogo wameshaanza kuzungukwa zungukwa na viumbe fulani (viburudisho wenyewe wanaviita).Ghafla huko kwenye dansini floo Dijei akaweka “Hapo vipii..” ya huyu mwanabongofleva mnayemuita Profesa nanihii…Jei.

Jamaa wawili wakaibuka zao kwenye dansin floo kuyarudi mangoma, hapo ndipo ishu iliponoga sasa jamaa walikuwa wanakata zao Tusker na Nondo sijui ndio ubrazameni wenyewe jamaa (Rwego) kachomoka kaunta fasta kaibuka chukua zake hiyo nanihii ya chupa ya kijani… Bavaria na ufunguo wa gari kaenda kuyarudi.

“Kinda gateni mpaka chuoni kikuu longi taimu kwa machizi na masista duu…” ndivyo anavyokwenda sambamba na vesi za huo mziki, huku akiwa katikati kabisa ya masela kibao(hiyo ni naiti kali). Wanaomfahamu wanapigwa butwaa kwa jinsi anavyonyanyua juu Bavaria na ufunguo wa gari hawaelewi elewi. Wengine wanafikiri labda kashinda kwenye promosheni hapo nje dakika kadhaa zilizopita ndio anasherekea.
Lakini jamaa zake wanaoendelea na kilaji mezani wanamsanifu tu “Cheki jamaa ayah…! Kashaachana na hii sasa ana Bavaria siumeona mikono ile? Mwingine anayeonekana kumfahamu vilivyo akadakia “Hamna hiyo atakuja kuinywa sianamtaka Eliza pale (ananyooshea kidole meza nyingine) anataka aone kwamba na yeye matawi halafu na usafiri haumpigi chenga”.

Duh! Hivi kumbe bado hizi staili bado zipo? Duh! Ndio matatizo ya kuvamia jiji la watu sasa hata kama umepiga skuli bado wakuja tu.

Lakini wanangu ebu ngoja kidogo tuachane na Rwego tucheki na ishu zingine huko Dasilamu mjini. Nimeskia kuna ‘Maprofesa’ wamemwaga wino tayari kutoa ‘lekcha’ Jangwani.

Huyo bosi nimebonyezwa anaitwa Condic Dusan na msaidizi, Solokoviskiii na naskia wameshapewa rungu na tayari kufanya baadhi ya ishu ili kuhakikisha neksti raundi ya Ligi Kuu kinaeleweka Jangwani. Lakini Wekundu wataachia hilo kopo la ubingwa? Simo!

Kitendo cha Yanga kuleta makocha hao raia wa Serbia ni changamoto kubwa katika soka la Tanzania ambayo inastahili kuigwa na klabu zote za Ligi Kuu ili kuinua kiwango na kubadili taswira ya soka la Bongo.

Kama ilivyo kwa wadau wengine wa Bara, naungana na wadau wengine ambao wamekuwa wakisema kwamba huenda kukawepo na changamoto kubwa kwenye Ligi haswa kutokana na uzoefu, rekodi na utaalam wa makocha hao ambao wametamba na klabu kadhaa maarufu za Afrika ya Kati na Magharibi.
Si suala la kupongezwa tu. Uongozi wa Yanga unapaswa kuacha ubabaishaji nikiwa namaanisha kwamba unapaswa kutoa ushirikiano na sapoti ya kila aina kwa makocha hao.Vinginevyo muda si mrefu watapotea tena kama walivyopotea wengine, wala hakuna atakayeshangaa.

Hao jamaa msiwageuze wadoli kwamba mmewaleta ili kujionyesha kwamba mnaweza au mna jeuri ya fedha haisaidii!

Hii kauli aliyokuwa akipenda kuitumia huyu kocha Mserbia Sredjoviv Milutin ‘Micho’ kwamba Yanga ina baadhi ya viongozi ambao ni “Leaders of Conflict and gate collection (viongozi wa migogoro na mapato ya milangoni)” ndio moja kati ya sababu zilizomfanya akashindwa kufanya mambo yake naamini bado ina ukweli ndani yake.

Sishawishiki kuamini kwamba hali hiyo imekwisha ndani ya Yanga kwa kipindi hiki cha miezi michache tangu Micho ambaye alikuwa amezoea mazingira ya ‘kiswahili’ atimke Jangwani.

Viongozi wenyewe kwa wenyewe wanapaswa kuhakikisha kwamba kila mmoja anawajibika kwa nafasi yake na hata kama ikiwezekana ziwepo kamati ndogondogo za watu makini ambao watapewa majukumu ili kuwarahishia kazi hao makocha wa kigeni.

Kuwa mzungu si kujua kila kitu, na si lazima kila kitu afanye Mwenyekiti au Katibu huu ni wakati wa mgawanyo wa majukumu. Si mtu unakaa Dar es Salaam wiki nzima wala hujui ilipo timu halafu unaskia inacheza Mbeya jumamosi unakwea pipa Ijumaa kwenda kusimamia mapato na baadae unapotea kwenye mazingira ya utatanishi.
Ebwana habari ndio hiyo! Mida basi masela.

No comments: